Tarehe : March 5, 2019, 2:14 p.m.
Katika kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Wanawake kutoka Wizara za Madini, Nishati na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), leo Machi 5, wamefanya Matendo ya Huruma kwa kuwatembelea watu wenye mahitaji maalum na kutoa mahitaji mbalimbali ya kijamii.
Vituo vilivyotembelewa na wanawake hao ni Shule ya watoto wasioona na kituo cha watu wazima wasioona vilivyopo katika Kata ya Buigiri, Halmashauri ya Chamwino jijini Dodoma kwa lengo la kujumuika pamoja kabla ya kilele cha maadhimisho hayo ambayo hufanyika tarehe 8 Machi, kila mwaka.
Akizungumza kwa niaba ya ujumbe huo mara baada ya kuwasili katika shule ya watoto wasioona, Afisa Utumishi kutoka Wizara ya Madini anayeshughulikia masuala ya wanawake Remida Ibrahim, amesema kutokana na wanawake kuguswa zaidi na masuala ya kijamii ndio sababu iliyopekea ujumbe huo kufika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa mahitaji mbalimbali ili yaweze kuwasaidia watoto hao.
Remida amewaasa wanafunzi hao ambao asilimia tisini na tano wana ulemavu wa kutokuona kusoma kwa bidii ili kujikwamua na maisha yao ya baadaye na kuwataka kuelewa kuwa Serikali inatambua uwepo wao na kwamba iko bega kwa bega katika kuhakikisha inachangia katika kutoa elimu bora.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule hiyo, Historia Mputa, ameushukuru ujumbe wa wanawake kutoka katika makundi hayo kwa kutoa kipaumbele kwao na kuamua kutembelea kituo hicho na kueleza, “vituo vya watoto wenye mahitaji maalum ni vingi sana lakini mmeona vema kututembelea mahala hapa tunashukuru sana”, amesisitiza.
Baada ya kukamilisha shughuli ya kukabidhi zawadi katika kituo hicho, ujumbe hao ulihamia katika kituo cha wasioona watu wazima ambapo walipata fursa ya kusikia historia fupi ya kituo na kusikiliza kero mbalimbali zinazokikabili kituo hicho na baadaye kukabidhi bidhaa zitakazosaidia katika kupata mahitaji kwa siku kadhaa.
Akizungumzia uanzishwaji wa kituo hicho, Mwenyekiti Msaidizi wa kituo hicho Yusuph Matando, amesema kituo hicho kilianzishwa mnamo mwaka 1992 na Mwalimu Keneth D. Mwanampalila na kufadhiliwa na Kendall Lee wa nchini Uingereza kwa lengo la kuwasaidia watu wasioona kujipatia mahitaji yao kwa shughuli za kilimo cha mbogamboga badala ya watu hao kuombaomba mtaani.
Yusuph amebainisha changamoto zilizopo kituoni hapo kuwa ni hicho kuwa ni pamoja kutokufikiwa na huduma ya umeme ,ugumu katika upatikanaji wa mbegu, uhaba wa mipira ya maji kwa ajili ya kumwagilia bustani zao pamoja na maji yanayopatikana katika kisima hicho kutokutosheleza mahitaji ya kijiji.
Siku ya wanawake duaniani huadhimishwa tarehe 8 Machi ya kila mwaka ikilenga kusisitiza kujenga mshikamano wa wanawake wote duniani, kuelimisha kuhusu jitihada zinazofanywa na serikali na taasisi zisizo za serikali katika kuwaendeleza wanawake na kuhamasisha utekelezaji wa Sera na mipango ya Serikali yenye lengo la kudumisha amani, usawa na maendeleo.
Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Mwaka 2019 ni “ Badili fikra, fikiria usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu’’
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.