Tarehe : Oct. 18, 2018, 8:36 a.m.
Na Nuru Mwasampeta,
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko amezitaka halmashauri za wilaya kufanya kazi na wizara ili kuweza kutatua changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao kabla hazijasababisha madhara makubwa kwa jamii.
Mmoja kati ya wafanyakazi wa mgodi wa uchimbaji wa madini ya mchanga akielezea jambo kwa Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko(wa pili kulia) alipotembelea mgodi huo[/caption]
Aliyasema hayo mwanzoni mwa wiki alipofanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Pwani wilaya ya Mkuranga alipofika ili kukagua shughuli za uchimbaji wa mchanga unavyoendelea pamoja na kukagua namna ya ulipwaji wa mirabaha ya Serikali inavyofanyika.
Akizungumza katika kikao baina yake na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Hassan Sanga, Biteko alisema “Sisi ni wamoja hivyo tufanye kazi kwa pamoja, tunajifunza pamoja ili tuamue kwa pamoja”.
“Tunatamani mambo mengi yaishie huku chini lakini endapo kuna masuala yanahitaji msukumo wa wizara ninyi mtueleze” alisistiza Biteko.
Aidha, Biteko aliwataka viongozi wa wilaya ya Mkuranga kuhakikisha tozo zinazotozwa na halmashauri hiyo ziwe ni zile zinazokubalika kisheria ili kupunguza migogoro midogomidogo baina ya Serikali na wachimbaji lakini pia kuwasaidia wachimbaji ili waweze kukua na kuongeza kipato chao.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga alibainisha uwepo wa utoaji wa leseni bila ofisi yake kushirikishwa na hivyo kuwawia ugumu pindi wanapotakiwa kuchukua hatua za kuzuia eneo husika kufanyika shughuli za uchimbaji. “Mchanga unachimbwa kiholela ukiuliza wanasema wanavibali kutoka wizara ya ardhi, madini lakini pia wana vibali kutoka Nemc, tunashindwa kuwachukulia hatua.
Akizungumzia suala hilo Biteko alisema, mmiliki yeyote wa leseni ya madini hatakiwi kuanza kazi pasipo kutoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ambaye atapaswa kukutambulisha katia ngazi zote mpaka katika uongozi wa kijiji leseni yako.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko akitembea kuelekea eneo ambako uchimbaji wa mchanga unafanyika.[/caption]
Aidha aibainisha kuwa maeneo ya jeshi, vyanzo vya maji, maeneo ya hifadhi hayaruhusiwi kutolewa leseni lakini pia aliwataka viongozi hao wa wilaya kusema maeneo wanayodhani hayapaswi kutolewa leseni na kwamba wizara itatii kwa kutokutoa leseni kwa maeneo hayo.
Pia alielezea mamlaka ya wilaya kuwa inauwezo wa kuomba leseni zote zilizoombwa kwa kipindi Fulani ili kujiridhisha kama maeneo hayo yanaweza endeleza shughuli za uchimbaji na kama ni vinginevyo leseni zinafutwa.
Pamoja na hayo, Biteko aliutaka uongozi wa wilaya kuwalea wachimbaji na kuondokana na urasimu usiokuwa na sababu, “tuwahurumie watu, Urasimu usiokuwa na sababu sisi wizara ya madini tunasema hapana.” Alisema Biteko.
Biteko alitanaibisha kuwa, wawekezaji wanatumia pesa nyingi kuwekeza kwenye uchimbaji na wengine wana mikopo katika mabenki hawalali vizuri hivyo tuwasaidie ili waweze kufanya kazi zao kwa utulivu na kupata kile wanachotarajia.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.