[Latest Updates]: Wachimbaji Wadogo wa Madini Watakiwa Kuchamgamkia Fursa za Utafiti

Tarehe : Sept. 22, 2023, 8:58 a.m.
left

 

●Tafiti za awali za jiolojia  zimefanyika kwa asilimia 97

●Utafiti wa Jiokemia asilimia 23

●Utafiti wa Jiofizikia asilimia 16

Wachimbaji wa Madini wametakiwa kuchangamkia fursa za taarifa za utafiti wa Madini zinazofanywa na Wizara ya Madini kupitia Taasisi  ya Jiolojia na Utafiti wa Madini  Tanzania (GST) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ili kuchimba kwa tija.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 22 Septemba 2023 na Mjiolojia Mwandamizi Deogratius Oreku  wakati akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa  Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe alipotembelea Banda la Wizara ya Madini na Taasisi zake  katika maonesho ya sita (6) ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.

Mapema baada ya kupata taarifa za maendeleo ya Sekta ya Madini , Naibu Waziri alitaka kufahamu kuhusu taarifa za utafiti  ili kuwasaidia wachimbaji wadogo katika uchimbaji Madini.

Akifafanua kuhusu taarifa za utafiti zinazotolewa na Wizara kupitia machapisho mbalimbali , Oreku amesema kuwa Wizara ya Madini kupitia kitabu cha Mwongozo wa Wachimbaji Madini Wadogo kimekuwa msaada mkubwa kutokana na taarifa zilizochapishwa kuhusu hatua za utafutaji Madini.

Sambamba, na mwongozo huo  Wizara kupitia Taasisi zake imefanya utafiti wa kina katika maeneo saba yaliyotengwa kwa ajili ya uchimbaji mdogo ambapo utafiti wa  awali wa jiolojia umefanyika kwa asilimia 97, Jiokemia asilimia 23 na Jiofizikia asilimia 16  hivyo wachimbaji wadogo wanaweza kutumia taarifa hizo ili waweze kuchimba kwa urahisi na uhakika.

Maonesho ya sita ya Tekinolojia ya Madini kwa mwaka 2023 yanaongozwa na kaulimbiu inayosema " Matumizi Sahihi ya Teknolojia katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi mazingira"

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals