[Latest Updates]: Jengo la Wizara ya Madini kukamilika ifikapo Januari 4, 2019

Tarehe : Nov. 29, 2018, 9:19 a.m.
left

Na Rhoda James, Dodoma

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ameagiza Kampuni ya Mzinga Holding Co. Ltd kukamilisha ujenzi wa Jengo la Wizara ya Madini ifikapo Januari 4 mwaka 2019.

Ametoa agizo hilo jana tarehe 4 Desemba, 2018 alipofanya ziara ya kukagua eneo la ujenzi wa ofisi za Wizara lililopo Ihumwa Jijini Dodoma akiambatana na viongozi wengine waandamizi wa wizara.

Muonekano wa eneo la ujenzi wa Jengo la Wizara ya Madini.[/caption]

Kairuki alibainisha kuwa baada ya sikukuu za mwisho wa mwaka, viongozi wote watatakiwa kuhamia katika eneo hilo kutokana na ukweli kuwa ifikapo Januari 4 jengo hilo litakuwa limekamilika.

Aidha, Waziri Kairuki ameshauri kuwa wakati wanaendelea na maandalizi mengine waendelee na manunuzi ya vifaa, na vifaa hivyo lazima viwe vya viwango ikiwezekana watumie dealers ambao ni wakubwa na wa uhakika.

Kwa upande wake, Mhasibu Mkuu wa Wizara, Anthony Tarimo alisema kuwa pesa kwa ajili ya ujenzi huo ipo, wao wanachohitaji ni kujua mkataba ukoje na guarantee ili pesa kwa ajili ya ujenzi huo itolewe.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Issa Nchasi ameeleza kuwa wamejiandaa kikamilifu ili kusimamia ujenzi wa Jengo hilo na atateua watu ambao watafutilia kwa ukaribu shughuli za kila siku za ujenzi wa Jengo hilo.

Vile vile, Mwakilishi wa Kampuni ya Mzinga Holding Co. Ltd, Mhandisi Hagai Mziray amesema wataanza maandalizi ya ujenzi wa Jengo la Madini mapema tarehe 5 Decemba, 2018 na watafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kuwa wanakamilisha ujenzi kwa wakati.

Mziray ameongeza kuwa Kampuni yao inao uzoefu wa kutosha katika masuala ya ujenzi kwani wamejihusisha na ujenzi wa majengo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Manispa ya jiji Dodoma, Hosipitali ya Makole, Hosipital ya Mkoa wa Morogoro pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi.

Kwa sasa Wizara ya Madini inatumia Ofisi za Wakala wa Jiologia Tanzania (GST) zilizopo Mjini Dodoma.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals