[Latest Updates]: Madini Kuweka Mikakati Shirikishi Uwekezaji Sekta ya Madini

Tarehe : Nov. 23, 2023, 3:02 p.m.
left

# Kushirikiana na Makampuni bingwa ya Ushauri nchini kuitangaza sekta ya madini

# Wizara ya Madini kufungua Dawati maalum la Uwekezaji TIC

Kufungua kiwanda cha uchenjuaji kitakacho hudumia  Ukanda wa Sub Sahara Afrika

Wizara ya Madini imepanga kuweka mikakati shirikishi  ya uwekezaji katika Sekta ya madini itakayowavutia na kuwanufaisha wachimbaji wadogo,wa kati na wakubwa.

Hayo yamebainishwa Novemba 21, 2023  na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali wakati akizungumza na uongozi wa kampuni ya BHP na Lifezone katika mkutano wa biashara  baina ya Tanzania na Uingereza unaoendelea jijini London.

Sambamba na hapo, amesema wizara ya madini itaandaa mpango wa mafunzo maalum yaani Apprenticeship Program katika maeneo kazi kwa maafisa ili kuongeza ujuzi na maarifa kwenye mnyororo mzima wa uwekezaji ndani na nje ya nchi.

Mahimbali ameongeza kuwa , wizara ya madini kwa kushirikiana na kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) itafungua Dawati maalum la  uwekezaji kwa ajili ya kuratibu shuguli za  uwekezaji ndani ya sekta ya madini.

Akielezea kuhusu ujenzi wa kiwanda cha uchenjuaji madini mkakati, Mahimbali ameeleza  kuwa Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya BHP Group Limited na Lifezone Metals kupitia kampuni tanzu ya Tembo Nickeli imepanga kujenga kiwanda kikubwa nchini Tanzania cha uchenjuaji madini mkakati yatakayochimbwa katika nchi zilizo Ukanda wa Sub Sahara Afrika.

Akiwa ameambatana na wataalam kutoka wizara ya madini, Mahimbali amesema kuwa Wizara ya Madini imeridhishwa na mwamko ulioneshwa na wawekezaji wa nchini Uingereza na kuahidi kutoa kushirikiana mzuri  kwa faida ya nchi zetu.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals