Tarehe : Nov. 23, 2023, 3:02 p.m.
# Kushirikiana na Makampuni bingwa ya Ushauri nchini kuitangaza sekta ya madini
# Wizara ya Madini kufungua Dawati maalum la Uwekezaji TIC
Kufungua kiwanda cha uchenjuaji kitakacho hudumia Ukanda wa Sub Sahara Afrika
Wizara ya Madini imepanga kuweka mikakati shirikishi ya uwekezaji katika Sekta ya madini itakayowavutia na kuwanufaisha wachimbaji wadogo,wa kati na wakubwa.
Hayo yamebainishwa Novemba 21, 2023 na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali wakati akizungumza na uongozi wa kampuni ya BHP na Lifezone katika mkutano wa biashara baina ya Tanzania na Uingereza unaoendelea jijini London.
Sambamba na hapo, amesema wizara ya madini itaandaa mpango wa mafunzo maalum yaani Apprenticeship Program katika maeneo kazi kwa maafisa ili kuongeza ujuzi na maarifa kwenye mnyororo mzima wa uwekezaji ndani na nje ya nchi.
Mahimbali ameongeza kuwa , wizara ya madini kwa kushirikiana na kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) itafungua Dawati maalum la uwekezaji kwa ajili ya kuratibu shuguli za uwekezaji ndani ya sekta ya madini.
Akielezea kuhusu ujenzi wa kiwanda cha uchenjuaji madini mkakati, Mahimbali ameeleza kuwa Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya BHP Group Limited na Lifezone Metals kupitia kampuni tanzu ya Tembo Nickeli imepanga kujenga kiwanda kikubwa nchini Tanzania cha uchenjuaji madini mkakati yatakayochimbwa katika nchi zilizo Ukanda wa Sub Sahara Afrika.
Akiwa ameambatana na wataalam kutoka wizara ya madini, Mahimbali amesema kuwa Wizara ya Madini imeridhishwa na mwamko ulioneshwa na wawekezaji wa nchini Uingereza na kuahidi kutoa kushirikiana mzuri kwa faida ya nchi zetu.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.