Tarehe : Oct. 18, 2018, 8:29 a.m.
Na Greyson Mwase,
Tarehe 19 Oktoba, 2018 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo alifanya ziara katika Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kabulo (Kabulo Coal Mine) uliopo katika eneo la Kabulo lililopo katika wilaya Songwe mkoani Songwe na Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira (Kiwira Coal Mine) iliopo katika Wilaya ya Ileje mkoani Mbeya. Mara baada ya kufanya ziara katika migodi husika, alizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira lengo likiwa ni kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Akizungumza katika mkutano wa wafanyakazi alisema kuwa, kwa sasa Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya kutoka Kabulo hadi Kiwira itakayotumika kwa ajili ya usafirishaji wa makaa ya mawe pamoja na kuhakikisha inalipa stahili za wafanyakazi mara baada ya taratibu kukamilika. Katika hatua nyingine, Nyongo aliwataka watumishi kufanya kazi kwa ubunifu na kusisitiza kuwa Wizara ya Madini itahakikisha wanafanya kazi katika mazingira mazuri.
Wafanyakazi wa Mgodi wa Kiwira walimpongeza Naibu Waziri Nyongo kwa kazi kubwa ya kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wa madini nchini pamoja na Taasisi zilizopo chini ya Wizara.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.