[Latest Updates]: Nyongo akagua miradi ya maendeleo jimboni kwake Maswa

Tarehe : March 10, 2019, 2:21 p.m.
left

Katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi na utekelezaji wa ahadi za chama kwa wananchi, Naibu Waziri wa Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki Stanslaus Nyongo leo amekagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika jimbo lake.

Nyongo alitembelea mradi wa ujenzi wa shule unaoendelea katika kata ya Nyalikungu na kuagiza shule hiyo ya  msingi ianze kupokea wanafunzi kuanzia mwezi huu ili kuwapa nafuu wanafunzi wanaotembea mwendo mrefu kutafuta elimu.

Aidha, Nyongo ameelekeza mwenge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakapopita katika wilaya ya Maswa, ndipo shule hiyo ifunguliwe rasmi ili kuruhusu masuala mengine ya kimaendeleo kutekelezwa.

Mara baada ya kukamilisha ukaguzi katika eneo hilo, Nyongo alielekea katika kijiji cha  ambako alikagua maendeleo ya ujenzi wa zahanati ambao haukuwa wakuridhisha aidha, alitembelea hospitali ya Wilaya ya Maswa kujionea eneo lililopendekezwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto ambalo mchakato wa ujenzi na upatikanaji wa pesa umekamilika.

Akizungumzia changamoto wanazokutana nazo katika eneo hilo la shule, Diwani wa Kata ya Nyalikungu, Joseph Bundara, alisema ni kutokuwa na barabara, huduma ya maji, umeme pamoja na ombi lakujengewa nyumba ya mwalimu ili kuishi karibu na mazingira ya shule.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi wa shule iliyopo katika kata hiyo ya Nyalikungu Katibu wa CCM wilaya ya Maswa Mwl. Mathius Filagisa alimtaka Diwani wa kata hiyo kuhakikisha wakati wa ziara za viongozi wa juu wa Chama na CCM viongozi wote na watendaji wote wa Serikali wawepo katika ziara na mikutano   ili kujibu hoja zitakazoibuka wakati wa mikutano hiyo.

Tunatekeleza Ilani ya CCM kuleta makaimu kwenye ziara za waheshimiwa haifai mjitahidi mwaunge mkono viongozi wenu wakati wa utekelezaji wa majukumu yao wawapo majimboni” alikazia.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals