[Latest Updates]: Bilioni 205 za Dhihirisha “Utakwimu” wa Biteko

Tarehe : Dec. 8, 2019, 8:31 a.m.
left

Issa Mtuwa – “WM” Nzega

Waziri wa Madini Doto Biteko amesema ataendelea kuongea kwa namba (takwimu) badala ya maneno huku akitamba kuwa wizara yake itavuka malengo ya makadirio ya makusanyo ya fedha zilizopangiwa na wizara yake kukusanya ambayo ni bilioni 475 katika mwaka wa 2019/20 huku akibainisha kuuwa ndani ya miezi 5 tu teyari wizara yake imeshakusanya bilioni 205.

Ameyasema hayo leo tarehe 7/12/2019 Wilayani Nzega alikokwenda kukabidhi Leseni 11 kwa vikundi 10 vya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu. Ameongeza kuwa kuongea ongea hakusaidii zaidi ya kufanya kazi na ukifanya kazi acha namba zikusaidie kueleza unachokifanya.

Pamoja na kukabidhi leseni hizo, Biteko ametoa masherti kwenye eneo moja la uchimbaji aliloliwekea mashaka kuhusu usalama wake kutokana na hali yake huku akiagiza kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya chini ya mwenyekiti wake ambae pia ni Mkuu wa Wilaya Godfrey Ngupula  kuhakikisha utaratibu wa usalama umezingatiwa kabla ya kuanza kuchimba.

Vikundi vilivyokabidhiwa leseni hizo ni pamoja na; Msilale Miners Group, Jimbo la Nzega Vijijini, Undomo Miners Group, Hapa Kwetu Group, Umoja wa Wachimbaji Mwanshina, Mkombozi Mining Group, Imalamakoye Miners Group, Salama Miners, Makalanga Minerals Group na Nzega Miners Association.

Biteko amesema uthubutu wake na viongozi wenzake wa wizara nzima ndio unaopelekea kuiweka sekta ya madini kwenye mwendo “mdundo” huku akiahidi yeyote anayetaka kurudisha nyuma mwendo huo hatokubaliana nae.

Ameongeza kuwa, mara kwa mara halali usiku kwa ajili ya kupokea simu za wananchi wakimpa taarifa za utoroshaji wa madini na taarifa mbalimbali. Hata hivyo amesema anakerwa na vitendo vya uchonganishi kwa kutoa taarifa za uongo huku akiwaomba wananchi kutoa taarifaa zenye ukweli na usahihi ili kulisaidia tafia.

“Madini haya si yangu mimi wala ya Rais John Pombe Magufuli, ni madini ya Watanzania na sote tunawajibu wa kuyalinda, kazi yangu ni kusimamia maekezo ninayopewa na Mhe. Rais na kuhakikisha sekta hii inachangia kwenye pato la taifa kama inavyostahili. Narudia tena, anae stahili sifa katika haya yote yanayofanyika kwenye madini sio Mimi Doto Biteko, anaye stahili sifa na pongezi zote ni Rais John Pombe Magufuli kwani yeye ndiye anaye elekeza na mimi ni msimamizi tuu wa kutekeleza yale anayo yaagiza.”. Alisema Biteko.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Leseni kutoka Tume ya Madini Mhandisi Yahaya Semamba amewaambia wanavikundi waliopatiwa leseni kuwa pamoja na kupatiwa leseni hizo wanapaswa kuzingati masherti ya leseni hizo na kwamba watakao kiuka watawafutia leseni yao. Miongoni mwa masherti hayo ni kuhakikisha ulipaji wa maduhuli ya serikali, kutunza mazingira, kuzingatia usalama na masherti mengine yote.

Akiongea kwa niaba ya wanavikundi wenzake waliokabidhiwa leseni Aluna Mgalula amemshukuru Waziri wa Madini na Mkuu wa Wilaya kwa kuwaondelea kero yao ya kupatiwa leseni. Ametoa ushuhuda wa namna alivyokuwa anamsumbua waziri Biteko kwa kumpigia simu hata usiku wa manane huku akipokea na kumsikiliza.

Mwenyekiti wa wachimbaji wadogo wilayani Nzega ametoa pongezi kwa serikali na wizara ya madini huku akimshukuru waziri Biteko kwa namna anavyo wasaidia wachimbaji wadogo katika kuwapatia maeneo mbalimbali na kuwafanya wachimbaji kuwa na utulivu katika kazi zao.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals