[Latest Updates]: Biteko akalipia ajali maeneo ya wachimbaji wadogo wa madini

Tarehe : Dec. 5, 2019, 10:26 a.m.
left

Na Nuru Mwasampeta

Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko amewataka wachimbaji wadogo wa madini kuzingatia uchimbaji salama ili kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara katika maeneo ya migodi. Ametanabaisha kuwa akifa mtanzania mmoja huyo Mtanzania ni muhimu kuliko mgodi wote, ‘kuliko mtanzania mmoja afe ni bora huo mgodi usiwepo’.

Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi (aliyesimama) akieleza jambo mbele ya Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (Kushoto) alipofika ofisini kwake kuelezea uwepo wake katika wilaya hiyo.[/caption]

Aliyasema hayo leo tarehe 04 mwezi Januari alipokuwa akifungua mafunzo ya wachimbaji wadogo katika eneo la uchimbaji mji wa Buhemba wilayani Butiama mkoani Mara inayoendelea kwa siku mbili.

Biteko alibainisha kuwa, Buhemba ni eneo linaloongoza kwa ajali kwenye migodi, huu mgodi ulifungwa na toka umefunguliwa kuna vifo vya wachimbaji kumi na mbili na majeruhi 20, Serikali haiwezi ikakubali hali hiyo iendelee “Mimi nakwambia mwenyekiti sitakubali hali hii iendelee mimi mwenyewe nitakuja kuufunga tena mgodi huu kama hali hiyo itaendelea hatuwezi kupoteza maisha ya watanzania” Biteko alisisitiza.

Biteko aliongeza kwa kusema, Serikali haiko tayari kuona kuwa watu wanaendelea kufa ndio maana imeamua kufika na kuandaa mafunzo  kwa ajili ya wachimbaji wadogo ili  waweze kufundishwa namna bora za uchimbaji salama na wenye tija.

Biteko alisema mafunzo hayo yanalenga kuwafundisha wachimbaji wadogo masuala ya uchimbaji salama, uchenjuaji, afya, na mazingira ya uchimbaji katika mkoa huu wa Mara.

Akiwapongeza wananchi na wachimbaji wadogo wa madini Buhemba, Biteko alisema kumetokea ugonjwa mmoja kwa watanzania wa kukwamisha mradi wa Serikali,  wananchi wanaanza vurugu na kudai fidia lengo ikiwa ni kukwamisha tu utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa watanzania lakini Buhemba mmeonesha ushirikiano mkubwa kutoka mwanzo mpaka mwisho wa utafiti.

Aidha, Biteko alimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa ushirikiano anaoufanya katika kusimamia shughuli za uchimbaji wa madini. Amesema mara nyingi wachimbaji wadogo wanakuwa kama watoto yatima lakini si kwa hapa Buhemba. Hawana mlezi, wanajiendesha wenyewe na wakati mwingine mamlaka za serikali zinajitokeza pindi matatizo yanapotokea lakini Mkuu wa wilaya amekuwa bega kwa bega.

Baadhi ya Wachimbaji wadogo waliohudhuria mafunzo yaliyoandaliwa kwa ajili yao yenye lengo la kuboresha sekta ya uchimbaji mdogo wa Madini yanayoendelea katika wilaya ya Butiama mjini Buhemba mkoani Mara.[/caption]

Aidha, Biteko aliwasihi wachimbaji wadogo wa Buhemba kuchangia kwa ukamilifu katika pato la taifa. Alisema wakati wote ukikutana na kesi ya utoroshwaji wa madini mhusika mkuu anakuwa ni mchimbaji mdogo. Aliendelea kwa kuwaeleza wachimbaji hao kuwa wamepata Rais ambaye anawapenda, anawajali anawadhamini, Rais anayependa  wachimbaji wadogo wahame kutoka kwenye daraja la chini na kuwa watanzania wanaofurahia maisha kwenye nchi yao  kwa kuthaminiwa na kuheshimiwa, “nilidhani zawadi pekee ambayo mngeipa Serikali na Rais wetu DKt ni nyie kusimamiana mkalipa kodi vizuri, mhame kwenye mfumo wa kukwepa kodi na kutorosha madini”. Biteko alisisitiza

Pamoja na hayo Biteko alibainisha kuwa, katika mkoa wa Mara wilaya inayoongoza kwa kulipa kodi ni wilaya ya Butihama, alisema kiasi cha milioni 57 za kitanzania zimelipwa kwa mwezi jana, hata hivyo aliwahimiza wachimbaji hao  kufanya zaidi ili kuipa serikali wajibu mkubwa wa kuwahudumia.

“Ninapima mapenzi ya Rais Kwenu, halafu ninapima kile mnachochangia ninyi kwenye pato la Taifa haviendani” Mimi nilidhani mtu anayekupenda nawewe unamlipa kwa kumpenda zaidi. Rais wetu anawapenda wachimbaji wadogo hataki mtangetange, mpeni sababu ya kuendelea kuwapenda, mpeni sababu ya kuendelea kuwahudumia, siku mtu akiwagusa Rais awateteee kutokana na kodi zenu”

Naomba sana muwe wazalendo, muwe waaminifu, ili mchango wenu katika sekta hii uweze kuonekana na kutumika katika maeneo mengine nchini. Ili Serikali iweze kuhudumia maeneo mengine kama vile elimu, afya, usafirishaji na mambo mengine ni kutoka katika kodi. Simamianeni ninyi kwa ninyi, onyanenyi ninyi kwa nini bora mtu mbaya bora ake nje ya sekta.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wachimbaji Wadogo Mkoa wa Mara (MAREMA) Dave Bita alitoa shukrani zake za dhati kwa serikali kwa kutupa jicho kwa wachimbaji wadogo kwa lengo la  kuwawezesha kuwa na uchimbaji wenye tija. Aliishukuru Serikali kwa kujipanga kuwajengea kituo cha mafunzo kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha masuala ya utafutaji na uchimbaji wa madini.

Ameishkuru Serikali kwa kuwasilisha taarifa ya utafiti ulioanza mwezi Oktoba 2016 kwa wachimbaji wa Butiama matokeo yatakayowapelekea kunufaika na uchimbaji wao.

Aidha, Dave amewataka wachimbaji wadogo kutengeneza mazingira ya kukubali kuwalipa posho viongozi wanaowasimamia katika shughuli zao vinginevyo wataendelea kugombana na viongozi hao siku kwa siku na hata kupelekea migogoro. Amesema wachimbaji wadogo hawako tayari kuwalipa viongozi wanaowasimamia katika maeneo ya uchimbaji.

Aidha, amewasihi wachimbaji wadogo kutumia mafunzo yanayotolewa kwa manufaa ameomba watoe ushirikiano kwa voiongozi watakaowachagua pamoja na kuwasihi kukitumia kwa manufaa kituo cha mafunzo kinachojengwa na serikali kwa ajili yao.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals