Tarehe : April 28, 2018, 2:31 p.m.
Serikali imesema itawachukulia hatua za kinidhamu watendaji wanaotumia madaraka yao vibaya kwa kuwanyanyasa wachimbaji wadogo wa madini nchini ili kujipatia kipato kinyume na taratibu.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (mwenye kipaza sauti) akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu kwenye machimbo ya Kitunda ya Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora. Biteko alifanya ziara kwenye machimbo hayo ili kujionea shughuli zinazoendelea sambamba na kuzungumza na wachimbaji.[/caption]
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko kwenye mkutano na wachimbaji wadogo wa madini katika machimbo ya Dhahabu ya Kitunda yaliyopo Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora.
Wakielezea changamoto zinazowakabili, wachimbaji wa machimbo hayo kwa nyakati tofauti walimueleza Biteko masikitiko yao juu ya unanyasaji wanayofanyiwa na baadhi ya Maafisa wa Serikali wasiowaaminifu wakiwemo Askari Polisi na Maafisa Madini.
Wachimbaji hao walisema kumekuwepo na tabia ya kushinikizwa kutoa rushwa ama kugawana faida kwa vitisho kuwa watazuiwa kuendelea kufanya shughuli zao kwenye maeneo yao.
“Kuna baadhi ya Maafisa Madini na Askari Polisi wamekuwa wakitulazimisha nao tuwape mgawo wa mawe tunayochimba vinginevyo watafukia maduara yetu,” alisema Alfred Kulwa mmoja wa wachimbaji kwenye machimbo hayo.
Kufuatia malalamiko hayo, Naibu Waziri Biteko alitoa onyo kwa watendaji wenye tabia hiyo kuacha mara moja na alimuagiza Afisa Madini kushirikiana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya husika kuhakikisha wanafuatilia suala hilo na watakaobainika hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
“OCD, tendeni haki, hawa wawe salama. Askari atakayebainika ananyanyasa mchimbaji madini achukuliwe hatua za kinidhamu haraka bila kuchelewa,” aliagiza Naibu Waziri Biteko.
Biteko alisema Afisa yeyote anayehitaji kujishughulisha na biashara ya madini aache kazi ili ajikite katika biashara hiyo na sio kutumia cheo chake kuwanyanyasa wachimbaji.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (mwenye kipaza sauti) akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu kwenye machimbo ya Kitunda ya Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora. Biteko alifanya ziara kwenye machimbo hayo ili kujionea shughuli zinazoendelea sambamba na kuzungumza na wachimbaji.[/caption]
Aliongeza kuwa hairuhusiwi Mtumishi wa Umma kutumia cheo kujinufaisha. “Marufuku watendaji wa Serikali ama wamiliki wa leseni za uchimbaji madini kutumia madaraka yao vibaya. Kama unataka ingia uchimbe mwenyewe. Serikali hii ya Awamu ya Tano inatutaka tuondoe manyanyaso,” alisema Biteko.
Biteko alisema mchimbaji atakayenyanyaswa atoe taarifa Polisi na pia amfahamishe kwa njia ya simu kuhusiana na manyanyaso hayo ambapo alitaja namba zake za simu ili kukitokea hali ya sintofahamu wasisite kumfahamisha.
Hata hivyo, Biteko aliwataka wachimbaji hao kuacha kuwasilisha taarifa za uwongo ikiwemo kusingiziana na mara zote wasimamie haki ili kuepusha migogoro baina yao na Serikali.
Imeandaliwa na:
Mohamed Saif,
Afisa Habari,
Wizara ya Madini,
5 Barabara ya Samora Machel,
S.L.P 2000,
11474 Dar es Salaam,
Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,
Barua Pepe: info@madini.go.tz,
Tovuti: madini.go.tz
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.