[Latest Updates]: Waziri Mavunde Aeleza Umuhimu wa Madini Bonanza

Tarehe : Oct. 19, 2024, 1:01 p.m.
left

Awahamasisha Watumishi kujiandikisha kwenye daftari la Wapiga Kura Serikali za Mitaa


GST  Yazoa Medali za kutosha

Madini Yanga Yanyakua Ubingwa

Dodoma

Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameeleza kuhusu umuhimu wa Madini Bonanza na kueleza kuwa limelenga kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano baina ya  Watumishi wa Wizara na Taasisi zake ili kuifanya Wizara kuwa familia moja.

Amesema hayo leo Oktoba 19, 2024 katika Viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlin – Miyuji jijini Dodoma, wakati akizungumza katika Madini Bonanza lililowajumuisha Watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake. 

" Ninawapongeza kwa bonanza hili kwasababu linatusaidia kukaa  pamoja, kufurahi na kufahamiana zaidi," amesema.

Aidha, amewasisitiza watumishi  kujenga utamaduni  wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao, na kuongeza," kama mnavyofahamu hivi sasa takwimu  zinaonesha kuna changamoto kubwa ya magonjwa yasiyoambukiza hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kufanya mazoezi,".

Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde amewahamasisha watumishi wa Wizara kujishiriki katika zoezi linaloendelea hivi sasa la kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa unaotarajia kufanyika mwezi Novemba mwaka huu.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Terence Ngole ameeleza kuhusu  mashindano ya michezo mbalimbali yaliyofanyika yakihusisha mpira ya miguu, pete, kamba, mbio za mita 100 na mita 400 ambapo  washindi mbalimbali wamepatikana kutoka Wizara na Taasisi zake huku Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania ( GST)  ikiondoka na medali  lukuki na makombe.

#MichezoniAfya
#MichezoniFuraha
#MichezoniAjira

#Vision2030: MadininiMaishanaUtakiri

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals