[Latest Updates]: Tanzania Yafungua Fursa Uwekezaji, Utafiti na Usafirishaji Madini

Tarehe : Oct. 19, 2023, 8:32 a.m.
left

#Umoja wa Ulaya, Tanzania kuingia mkataba wa kushirikiana kufanya utafiti wa kina

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven  Kiruswa amewakaribisha Wawekezaji kuja Tanzania kuwekeza katika Utafiti, Uchimbaji pamoja kujenga Viwanda vya kusafishia Madini, ili kuongeza thamani kabla ya kusafirishwa kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi.

Amesema kuwa Sera nzuri za Tanzania katika Uwekezaji wa Sekta ya Madini pamoja na mambo mengine imelenga kuleta manufaa kwa Nchi na pamoja Wawekezaji.

Aliyasema hayo Oktoba 18, 2023, Jijini Cape Town nchini Afrika Kusini, wakati akizungumza katika Mkutano wa Mawaziri uliolenga kujadili Utajiri wa Madini Mkakati na namna ya kuimarisha  Ushirikiano baina ya Nchi zenye utajiri huo na Nchi za Afrika, Mataifa yenye mitaji pamoja na Watengenezaji wa vifaa vinavyotokana na Madini Mkakati.

Dkt. Kiruswa alifafanua kuwa nchini Tanzania wapo Wawekezaji katika Madini ya Dhahabu(Barrick Co. Ltd) Graphite(Lindi Jumbo), Nickel (BHP) na Rare Earth Elements (Nguala REE project) miradi yote ikiwa katika hatua mbalimbali na kwamba Tanzania inakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika Sekta ya Madini. 

Vilevile, Dkt. Kiruswa aliongeza kuwa tayari Umoja wa nchi za Ulaya (EU) upo katika mpango wa kujadiliana na Tanzania na kuingia Mkataba wa Makubaliano ili kushirikiana kufanya utafiti wa kina.

Dkt. Kiruswa anaongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo wa kilele wa Madini Mkakati barani Afrika mwaka 2023 ukiwa na lengo la kuiweka Afrika kama kitovu kikuu cha Uwekezaji wa Madini Mkakati.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals