[Latest Updates]: Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Barrick Kujenga Barabara yan Km 73.9 Kiwango cha Lami

Tarehe : Nov. 5, 2024, 5:25 p.m.
left

●Kujengwa kwa miezi 27
●Barrick kufadhili kwa asilimia 100

 KAHAMA

Imeelezwa kwamba Kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Barrick inaendelea  na utekelezaji wa ujenzi wa Barabara ya Kahama hadi Bulyanhulu yenye urefu wa kilomita 73.9 kwa kiwango cha lami itakayogharimu kiasi shilingi zaidi ya bilioni 100.

Hayo yalielezwa hivi karibuni na Meneja wa Kampuni ya Barrick nchini Tanzania Melkiory Ngido wakati akizungumza katika mkutano na vyombo vya habari kuhusu Mpango wa Utekelezaji wa  Miradi ya Maendeleo yenye ubia na Serikali ya  Tanzania.

Akielezea kuhusu faida zitakazopatikana pindi mradi huo utakapo kamilika , Ngido alieleza kuwa wananchi wa Wilaya ya Kahama watapata fursa ya kusafirisha na kushiriki maendeleo ya kiuchumi pamoja na kusafiri kwa wepesi katika kutafuta huduma muhimu.

Ngido alieleza kwamba, pamoja na ujenzi wa barabara hiyo , tayari kampuni ya Barrick imetumia zaidi ya shilingi bilioni mbili katika ujenzi wa miundombinu ya barabara ikiwemo mitaro ya maji katika kijiji cha Kakola na Bushingwe na ujenzi wa Chuo cha Ufundi cha VETA cha Bunango, miradi ya afya na elimu katika vijiji vinavyozunguka mgodi Bulyanhulu

Naye , Mwenyekiti wa kijiji cha Ilogi Edward Shija alisema kuwa utekelezaji wa mradi  huo umeanza vizuri kwa kuwashirikisha wananchi kuanzia hatua za awali ambapo kukamilika kwa barabara hiyo  kutawezesha wananchi kufika  kwa haraka katika maeneo mengine yanayoungana na wilaya ya Kahama na vitongoji vyake  ili kupata huduma mbalimbali ikiwemo  Biashara , Afya na Elimu.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals