[Latest Updates]: Ujio wa Mwenyekiti  wa Bodi ya EITI Wazaa Matunda

Tarehe : June 22, 2024, 2:47 p.m.
left

Bodi ya EITI yaridhia Kikao cha Bodi kufanyika Tanzania 

Ushirikiano wa EITI na Tanzania kuimarishwa

Bodi ya Asasi ya Kimataifa ya (Extractive Industries Transparency Iniative - EITI) tarehe 18 - 20 Juni, 2024 ilifanya kikao chake cha 60 huko Geniva, Switzerland ambapo imeazimia kufanya Kikao chake cha Bodi ya Asasi hiyo nchini Tanzania mapema mwakani 2025 ambapo Mkutano huo umepangwa kufanyika Jijini Arusha.

Maamuzi hayo yamefanyika ikiwa ni miezi michache tu Mwenyekiti wa Bodi hiyo Retired Helen Clark pamoja na ujumbe wake walivyowasilia nchini kwa ziara Mwezi Aprili 2024  ambapo Mwenyekiti wa Bodi hiyo alifanya vikao mbalimbali na wadau kujadili utekelezaji wa shughuli za EITI hapa. 

Aidha Bi.Helen Clark alikutana na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko  na Waziri wa Madini Mhe. Antony Peter Mavunde, Kamati ya TEITI, Asasi za Kiraia na Makampuni ya Madini, Mafuta na Gesi Asilia.

Moja ya mambo muhimu yaliyozungumzwa ni Wizara ya Madini ikishirikiana na Asasi za Kimataifa ya EITI kutimiza kikamilifu mahitaji ya matakwa ya Kimataifa ya Uwazi na Uwajibikaji katika shughuli mbalimbali za Usimamizi wa Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia nchini. 

"Amesisitiza dhana ya kuweka uwazi taarifa na takwimu mbalimbali juu ya Sekta ya Uziduaji ni kuhakikisha kuwa Rasilimali hizo zinawanufaisha wananchi na kuahidi kuwa  TEITI itatoa ushirikiano katika kutekeleza Matakwa hayo".

Mapendekezo ya Kufanyika kwa Mkutano wa Bodi ya EITI ni kielelezo cha kuimarika kwa  Uwazi na Uwajibikaji katika usimamizi wa Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia hapa nchini. 

Mkutano huo utahudhuriwa na wajumbe zaidi 50 ikijumuishwa na Mwenyekiti wa Bodi Rt. Helen Clark, Sekretariati ya Asasi ya Kimataifa ya EITI na waalikwa mbalimbali kutoka nchi mbalimbali duniani.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals