[Latest Updates]: STAMICO Kinara wa Mageuzi, Rais Samia Aimwagia Pongezi, Yiabuka na Tuzo kwa Mara ya Pili

Tarehe : Aug. 28, 2024, 3:36 p.m.
left

● Yapongezwa utoaji wa gawio la bilioni 9 kwa Serikali 2018\19-2023\24

●Rais, Dkt.Samia aipongeza STAMICO kwa kukusanya bilioni 85 katika mwaka 2023/2024

● Yapata tuzo ya Ufanisi Katika Utendaji (Operational Excellence And Financial Performance )

Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amelipongeza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kwa mageuzi makubwa ya kiutendaji yaliyopelekea Shirika kuendesha miradi yake kwa faida kubwa.

Dkt.Samia amesema hayo leo Agosti 28, 2024 wakati akihutubia katika Kikao  Kazi cha Watendaji Wakuu na Wenyeviti wa Bodi wa Taasisi za Umma kinachoendelea mkoani Arusha.

Dkt. Samia amesema kuwa, STAMICO imefanya mageuzi makubwa yenye faida kwa Serikali  ambapo katika Mwaka wa Fedha   2018\2019  STAMICO iliweza kukusanya shilingi bilioni 1 na baada ya Serikali kupitia Msajili wa

Hazina  kuliwezesha Shirika  sasa linafanya mageuzi makubwa katika sekta ya madini nchini.

Rais Dkt.Samia ameeleza kuwa, mchango wa wachimbaji wadogo kwenye mnyororo mzima wa sekta ya madini umefikia asilimia 40 hii ni  kutokana na usimamizi mzuri wa STAMICO. 

Akielezea kuhusu gawio kwa Serikali , Dkt.Samia ameipongeza STAMICO kwa kutoa gawio la shilingi bilioni 9 kuanzia kipindi cha Mwaka wa Fedha 2018\19 hadi 2023\2024.

Nae , Msajili wa Hazina Tanzania Nehemia Mchechu amesema Sheria mpya inatungwa ili kusimamia Mashirika na Taasisi za umma katika kukuza ufanisi na uwajibikaji ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia  Hassan.

Kwa upande ,  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema Rais Dkt.Samia amefungua nchi katika fursa za kiuchumi na kidiplomasia hivyo ameyataka mashirika ya umma kutumia fursa hiyo kuimarisha na kufungua uwekezaji  ndani na nje ya nchi.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals