[Latest Updates]: Watumishi Madini Wampokea Katibu Mkuu Mpya Mahimbali

Tarehe : Feb. 28, 2023, 8:19 a.m.
left

Awaahidi Ushirikiano, akaribisha mazungumzo yenye kujenga Sekta

Rais Samia amteua Mhandisi Samamba kuwa Katibu Mtendaji Tume ya Madini

Naibu Waziri Dkt. Kiruswa apongeza Uteuzi wake

Dodoma

Watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake leo Februari 27, 2023, wamempokea Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Madini Kheri Mahimbali katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu.

Akizungumza na watumishi katika kikao kifupi baada ya kuwasili ofisini hapo, Mahimbali ameomba ushirikiano ili kuijenga sekta ya Madini na kueleza kuwa, mlango uko wazi kwa mazungumzo yatakayoongeza tija kwenye sekta.

" Mimi si mbobezi kwenye masuala ya madini lakini ninategemea kujifunza mengi kutoka kwenu na hivyo ninawaahidi ushirikiano tufanye kazi kama timu moja," amesema Mahimbali.

Awali, akizungumza katika kikao hicho, Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amemweleza Katibu Mkuu Mahimbali kuwa viongozi na watumishi wa wizara wako tayari kushirikiana naye kwa dhati kwa maendeleo ya sekta ya madini.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kiruswa amepongeza uteuzi wa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Yahya Samamba ambaye ameteuliwa na Rais Samia wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

" Katibu Mkuu, Samamba ni moja ya watendaji tunaovutiwa naye," amesema Dkt. Kiruswa.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals