[Latest Updates]: Biteko asema ufahari wa kiongozi uwe kwenye kuwatumikia Wananchi

Tarehe : March 15, 2019, 2:09 p.m.
left

Na Issa Mtuwa – Bukombe

Waziri wa Madini ambae pia ni Mbunge wa Bukombe Mhe. Doto Biteko amesema viongozi wa serikali wajibu wao mkubwa ni kuwatumikia wananchi, dhamana yao ya madaraka kama haina msaada kwa wananchi haina maana, yeye kama waziri na mbunge kama shida na matatizo ya wanchi wa Bukombe na sekta nzima ya madini atashindwa kuzitatua  haina maana ya uwepo wake na ndio maana anaumiza kichwa kila siku kuhakiksha sekta ya Madini inaleta tija kwa taifa huku pia wananchi wa Bukombe wanaozungukwa na Madini ya dhahabu pia wananufaika.

Biteko ameyasema hayo leo tarehe 02/03/2019 akihutubia wananchi kwa nyakati tofauti tofauti wilaya ya Bukombe katika siku yake ya kwanza ya ziara yake ya siku tatu katika mkoa wa geita ambapo pamoja na mambo mengine anasikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi na zinazo husu sekta ya madini.

“Rais Pombe Joseph Magufuli amekuwa akituambia mara kwa mara  nendeni mkawahudumie Watanzania muwaondolee kero, ule mfumo wa watu wakiwa ofisini anakuwa Boss Magufuli hataki mfumo huoo, anataka mabosi wawe wananchii, wananchi wasikilizwe kama wana jambo litatuliwe na kama haliwezekani waambiwe ukweli sio kudanganya” amesema Biteko.

Amesema Bukombe inautajiri wa madini ya dhahabu na endapo kila mmoja atajishugulisha katika kutafuta kwa kutumia fursa zilizopo maisha ya wana Bukombe yataboreka, ametoa wito kwa vijana, akina mama na kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi ajishugulishe.

Aidha, ameongeza kwa kusema wajibu alionao kama Waziri wa Madini ni kuhakikisha kodi na malipo mbalimbali yanayohusiana na madini yanalipwa tena kwa wakati, na jamii zinazo zunguka migodi zinachangia maendeleo ya wananchi hao kama sheria inavyo wataka.  

‘Msiwakamue sana hawa wawekezaji kwa sababu wanatumia fedha nyingi katika kuwekeza, sio kila shida ya kijiji, kata au wilaya mnakimbilia kwa mwekezaji wa mgodi hapaaaaaa….! lakini sizui kuwaomba msaada lakini kuwe na kipimo yale ya kisheria waacheni watekeleze ili wasipo timiza mimi nitawabana” aliongeza Biteko.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals