Tarehe : Feb. 7, 2024, 8 a.m.
Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeingia makubaliano na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake linaloshughulikia masuala ya Madini ya Metali, Gesi na Mafuta (JOGMEC) kufanya tafiti za Miamba na Madini nchini Tanzania.
Makubaliano hayo yamefikiwa kupitia kikao kilichofanyika tarehe 06 Februari, 2024 jijini Cape Town, Afrika Kusini baina ya taasisi ya GST na Shirika la JOGMEC.
Kwa upande wa Tanzania, imewakilishwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa, Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba na Mkurugenzi wa Kanzidata ya Taarifa za Madini Bi. Hafsa Maulid.
GST inashiriki Mkutano wa Mining Indaba unaoendelea jijini Capetown, nchini Afrika Kusini ulioanza tarehe 05 Januari na unategemea kufikia tamati tarehe 08 Februari, 2024.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.