[Latest Updates]: Wasanii wa Bongo Movie Wajifunza kwa Kina Kuhusu Sekta ya Madini

Tarehe : July 6, 2024, 11:04 p.m.
left

Dar es Salaam, 

Baadhi ya Wasanii wa filamu maarufu Bongo Movie wamepata fursa ya kujifunza kwa kina kuhusu sekta ya madini kupitia Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 

Wasanii hao, Sultan Mdima, Mwajuma Ramadhani, na Seif Mbembe wameonyesha shauku kubwa katika kuelewa mnyororo mzima wa shughuli za uchimbaji madini, mchango wa sekta ya madini kwenye uchumi wa nchi sambamba na namna wanavyoweza kutumia maarifa hayo katika kazi zao za sanaa. 

Aidha, wamepata maelezo ya kina kutoka kwa Wataalam wa Wizara ya Madini na Taasisi zake kuhusu mchakato ya uchimbaji, usafishaji, na kuongezea thamani madini mbalimbali kama vile Dhahabu, Almasi, Tanzanite na madini muhimu na mkakati. 

Sultan Mdima, mmoja wa wasanii waliohudhuria, amesema, “Ni muhimu sana kwetu kama wasanii kuelewa sekta mbalimbali za uchumi wa nchi yetu. Hii itatusaidia kuandaa kazi za sanaa ambazo sio tu zinaburudisha bali pia zinatoa elimu kwa jamii.”

Kwa upande wake, Mwajuma Ramadhani ameongeza, “Elimu hii imenifungua macho kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya madini. Ninashukuru kwa fursa hii na ninaamini itaongeza thamani katika kazi zetu za sanaa.”

Naye, Seif Mbembe ameeleza kuwa, “Nimejifunza mambo mengi mapya ambayo naweza kusema tunaweza  kuyatumia siku zijazo katika kutengeneza filamu na vipindi vya televisheni vinavyohusu maisha ya wachimbaji na sekta ya madini kwa ujumla, hii ni sekta muhimu sana”

Sanaa ya uigizaji na filamu ni daraja kati ya elimu na burudani katika sekta mbalimbali ikiwemo ya madini kwani zinaweza kuonesha hatua kwa hatua mchakato ya uchimbaji madini, kutoka kwa utafiti wa awali, uchimbaji, usafishaji, hadi usindikaji wa madini. Hii inaweza kusaidia watazamaji kuelewa jinsi madini yanavyopatikana na kuandaliwa kwa matumizi.

Pia, filamu zinaweza kuonesha jinsi sekta ya madini inavyosaidia jamii na kuchangia uchumi wa maeneo yanayohusika kwa kujumuisha fursa za ajira, maendeleo ya miundombinu, na changamoto za kiuchumi zinazoletwa na madini. Sambamba na kuangazia masuala ya haki za binadamu katika sekta ya madini, kama vile utumikishwaji wa watoto, 

Vilevile, filamu zinaweza kuonesha maendeleo ya kiteknolojia katika uchimbaji wa madini, kama vile matumizi ya mashine za kisasa, roboti, na teknolojia za usalama pamoja na kueleza jinsi madini yanavyosafirishwa na kuuzwa katika soko la kimataifa, na jinsi bei za madini zinavyoathiriwa na mambo ya kiuchumi na kisiasa duniani.

Kwa njia hizo, filamu zinaweza kutoa elimu muhimu kuhusu sekta ya madini, na kusaidia watu kuelewa na kushiriki katika mnyororo wa sekta ya madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals