[Latest Updates]: Mahimbali Apokea Taarifa Maendeleo ya Mradi wa Dhahabu Nyanzaga

Tarehe : June 24, 2024, 3 p.m.
left

Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali amepokea taarifa ya maendeleo ya mradi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu wa Nyanzaga uliopo Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza unao milikiwa kwa ubia kati ya Serikali kupitia Kampuni ya Sotta Mining Corporation Limited kwa asilimia 16 na Kampuni ya Perseus kutoka nchini Australia kwa asilimia 84.

Katika kikao hicho, Mahimbali ameipongeza Kampuni ya Persues Mining kwa wasilisho na taarifa iliyotolewa ambapo amewataka kuharakisha Mipango ya Kampuni hiyo ili mradi huo uweze kuanza kwa wakati.

"Naomba kuchukua fursa hii kuwapongeza kwa wasilisho zuri na niwaombe kuharakisha taratibu na mipango yenu ili mradi huu uweze kuanza kwa wakati kama ilivyopangwa na pia napenda kusema kwamba mradi huu ni mradi mkubwa na muhimu kwetu hivyo, nisisitize kwamba mradi huu uanze haraka," amesema Mahimbali.

Naye, Kamishna wa Madini Dkt. AbdulRahman Mwanga ameitaka Kampuni hiyo kuendelea na mipango wa utafiti na upembuzi yakinifu kwa ajili ya upanuaji wa mgodi huku shughuli za ujenzi wa mgodi zinaendelea kwa lengo la kuharakisha uzalishaji.

Naye, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Persues Mining, Matt Cavedom amesema, mradi wa uchimbaji madini ya dhahabu wa Nyanzaga unatarajiwa kuanza shughuli za ujenzi wa mgodi huo Januari, 2025 na kukamilika ndani ya miezi 24 ambapo utakuwa na uhai wa miaka 10.7.

Pamoja na mambo mengine, Cavedom amesema Kampuni ya Sotta Mining imekamilisha masuala yote yaliyopo kwenye Sheria ya Madini likiwemo suala la Ushirikishwaji wa Jamii Sehemu za migodi (Local Content) pamoja na mpango wa ufungaji wa mgodi pinda watakapomaliza shughuli za uchimbaji (Mining Closure).

Katika hatua nyingine, Cavedom meiomba Serikali kusaidia michakato mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa vibali kutoka Tume ya Madini ili kuongeza eneo la uchimbaji wa chini kwa chini (underground mining).

#InvestinTanzaniaMiningSector

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals