Tarehe : March 10, 2020, 9:43 a.m.
Na Nuru Mwasampeta, Dodoma
Waziri wa Madini, Doto Biteko leo Machi 10, 2020 amekutana na Wawekezaji wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Helium ya Noble Helium na kuitaka kuharakisha Utekelezaji wa mradi huo.
Biteko aliongeza kuwa hakuna serikali duniani isiyohitaji wawekezaji na hivyo basi kutokana na umuhimu na uhitaji wa wawekezaji nchini ni vema wawekezaji kwenda na kasi ya serikali husika ili kupelekea malengo yaliyowekwa na nchi kufikiwa ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa nchi.
Wawekezaji hao walipata leseni ya utafiti wa madini hayo katikati ya mwaka jana (2019) na hivyo kuamua kufika katika Ofisi ya Waziri Biteko ili kueleza hatua waliyofikia katika utafiti wa madini hayo.
Akizungumzia uhakika wa uwepo wa madini hayo nchini, Justyn Wood mmoja wa wajumbe kutoka kampuni ya Noble Helium, amesema kwa hatua za awali na kwa namna miamba ilivyokaa na jiolojia ya mahala wanapofanyia kazi wana uhakika mkubwa wa uwepo wa kiasi kikubwa cha madini hayo.
Wengine waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Viongozi Waandamizi wa wizara pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Dkt. Daniel Budeba.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.