[Latest Updates]: Kongamano la Kujadili Sekta ya Madini Kwenye Maonesho ya Pili ya Teknolojia na Uwekezaji Kwenye Madini Yanayoendelea Mkoani Geita

Tarehe : Sept. 26, 2019, 6:42 a.m.
left

Asteria Muhozya, Greyson Mwase na Boaz Mazigo,Geita

  • Asilimia 95 ya nchi nzima imefanyiwa utafiti wa jiolojia katika kiwango cha (scale) 1:125,000 na 1:100,000.
  • Asilimia 33 ya nchi nzima imefanyiwa utafiti na ramani zake bado hazijachapishwa kwa umma, ramani hizi zinasubiri taarifa za uhakiki ili kujiridhisha Zaidi kabla ya kuchapishwa.
  • Asilimia 62 ya nchi nzima imefanyiwa utafiti wa jiolojia na ramani zake kuchapishwa katika kiwango cha (scale) 1:125,000 lengo la taasisi ni kufanya tafiti nchi nzima katika kiwango cha 100,000.
  • Utafiti wa Jiokemia umefanyika kwa mikoa ya Mbeya, Songwe na Ruvuma kwa kushirikiana na  Taasisi ya China Geological Survey.
  • Utafiti wa Jiokemia na Jiofizikia umefanyika kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kusini kwa   kushirikana na Serikali ya Korea Kusini.

TAFITI NDOGO ZA UCHENJUAJI ZA HIVI KARIBUNI

  • Uchenjuaji wa madini ya graphite umefanyika na umekamilika
  • Taarifa ya Uchenjuaji wa dhahabu katika maeneo ya Msasa, forest, Mgusu, na Matabe, umefanyika na umekamilika. Taarifa inaenda sambamba na jiolojia (Bado uelimishaji)
  • Uchenjuaji wa madini ya dhahabu katika eneo la Nholi Bahi unaendelea.

FURSA ZINAZOTOLEWA NA GST KWA WACHIMBAJI WADOGO NA WAKUBWA KATIKA UTAFUTAJI NA UCHIMBAJI MADINI

  • Wachimbaji wanafaidika na machapisho yenye takwimu na ramani za kijiosayansi kwa ajili ya  kuwawezesha kuwekeza katika uchimbaji wa madini.
  • Wachimbaji wadogo wameendelea kupatiwa mafunzo ya uchimbaji wa madini
  • Ufundishaji wa uongezaji thamani, value addition kwa baadhi ya miamba na madini.
  • Huduma za maabara kwa ajili ya utambuzi/uchunguzi wa sampuli za madini na utafiti. Aina zote za madini zinaweza kutambuliwa na maabara ya GST.
  • Maabara ya uchenjuaji madini
  • Maabara ya kupima miamba,kokoto na udongo kwa ajili ya kutambua ugumu na ubora (geotechnical lab)

MATARAJIO

  • Kuendelea kufanya tafiti za kijiolojia kwa ajili ya kutambua miamba na madini, sehemu za kitalii, na madini mkakati (strategic metals)
  • Kundelea kutoa machapisho mbalimbali kwa ajili ya kukuza uelewa kwa wananchi na wadau wa sekta ya madini
  • Kuendelea kuwajulisha na kutoa elimu kwa wadau wa madini.

AMESISITIZA

  • Wadau wanaoguswa na Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Marekebisho yake ya Mwaka 2017 kuwasilisha data za utafiti GST.
  • Wachimbaji waendelee  kuitumia GST ktika shughuli zao za uchimbaji madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals