[Latest Updates]: STAMICO Yaongeza Mtambo Mpya wa Uchorongaji Kuimarisha Ufanisi kwa Wateja

Tarehe : Feb. 12, 2025, 4:51 p.m.
left

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeendelea kujiimarisha katika shughuli za Utafiti wa madini Nchini. Hii ni baada ya kununua Mtambo mwingine mpya wa kisasa wa Reverse Circulation (RC) kwa ajili ya shughuli za Uchorongaji miamba.

Mtambo huu (Rig) una uwezo wa kuronga hadi mita mia tatu (300) chini ya ardhi. Mbali na uchorongaji wa RC, mtambo pia una sifa ya uwezo wa kuchoronga staili nyingine za Rotary Air Blast (RAB) pamoja na Air Core (AC).
Ujio wa Mtambo huu mpya, umelifanya Shirika kuwa na jumla ya mitambo minne (4) ya kisasa ya Reverse Circulation (RC). 
     
Hakika, mtambo huu ni matunda ya matokeo makubwa ambayo Shirika linaendelea kufanya katika kandarasi za Uchorongaji miamba unaolenga tafiti za madini kwa Wachimbaji Wadogo, Wakati na Wakubwa hapa nchini. Shirika linaendelea pia kutoa huduma katika tafiti nyinginezo kama Joto Ardhi na Mafuta.        

Mtambo huu umewasili tarehe 9 February, 2025 katika mgodi wa ubia wa BUCKREEF na STAMICO uliopo katika kijiji cha Rwamgasa, Kata ya Katoro Mkoani Geita kwa ajili ya kusaidia shughuli za uchorongaji katika eneo la Uzalishaji (Pit) na utafiti maeneo ya jirani na mgodi.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals