[Latest Updates]: FEMATA watakiwa kuboresha sekta ya Wachimbaji Wadogo Nchini-Kairuki

Tarehe : Oct. 18, 2018, 8:38 a.m.
left

Na Rhoda James, Dodoma

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ameagiza Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji wa Madini (FEMATA) kuhakikisha kuwa wanakuja na Mikakati ya pamoja ya kuboresha utendaji kazi katika Sekta ya wachimbaji wadogo na kuweka mfumo bora wa kulipa Kodi za Serikali.

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki akihutubia Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini mbalimbali (hawapo pichani) jijini Dodoma alipokuwa kwenye Mkutano Mkuu wa Uchanguzi wa FEMATA jijini Dodoma tarehe 30 Oktoba, 2018.[/caption]

Waziri Kairuki, ameyasema haya jana tarehe 30 Oktoba, 2018 alipokuwa akifunga Mkutano Mkuu wa Uchanguzi wa Viongozi wa  FEMATA uliofanyika katika Hoteli ya Afrikan Dreams jijini Dodoma.

Kairuki amesema kuwa, Ukilinganisha wachimbaji wakubwa kwa wadogo nchini, wakubwa ni asilimia nne tu wakati wachimbaji wadogo ni asilimia 96 lakini ukitazama mchango wao kwa Pato la Taifa ni kinyume chake.

“Tunataka FEMATA mshiriki kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wanachangia kikamilifu katika Pato la Taifa,” alisema Kairuki.

Akizungumza katika Mkutano huo, Kairuki aliwataka wajumbe wote kutumia vyema furasa hiyo katika kujadili na kupanga mikakati itakayotekelezwa na kuimarisha Vyama vya wachimbaji wadogo Kimkoa (REMAS), FEMATA na hatimaye kuimarisha wachimbaji wadogo wa madini nchini.

Aidha, Waziri Kairuki amewapongeza FEMATA kwa kuandaa mkutano huo na kwa kutoa ushirikiano kwa Wizara ya Madini na kuhaidi kuwa atafanya kazi kwa karibu zaidi nao na nimatumaini yake kuwa ifikapo 2025 Sekta ya Madini itachangia ailimia isiyopungua10 ukilinganisha na mchango wa sasa ambao ni asilimia 4.8 kwa Pato la Taifa.

Akitoa pongezi kwa Uongozi wa FEMATA, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge alieleza kuwa ni matumaini yake kuwa wachimbaji na Wafanyabiashara wa madini wataendelea kulipa kodi zote serikalini kama inavyotakiwa.

Kwa upande wake, Rais wa Wachimbaji wa madini nchini John Bina amesema kuwa, atasimamia kikamilifu ulipaji kodi, uchimbaji salama na endelevu kupitia FEMATA.

Waliohudhuria mkutano huo ni Waziri wa Madini, Angellah Kairuki, Manaibu mawaziri wa Madini, Stanslaus Nyongo na Dotto Biteko, Mkuu wa Mkoa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Viongozi mbalimbali kutoka Serikalini ikiwa ni pamoja na Baraza la Taifa na Hifadhi ya Mazingira (NEMC), Wakala wa Usalama na Afya mahali pa Kazi (OSHA), Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Benki Kuu (BOT) pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wachimbaji na Wafanyabiashara wa madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals