[Latest Updates]: Wananchi Waonesha Shauku ya Kutumia Mkaa Mbadala wa Rafiki Briquettes

Tarehe : July 11, 2024, 3:26 p.m.
left

Wananchi wanaotembelea Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam wavutiwa na Mkaa Mbadala wa Rafiki Briquettes unaotengenezwa  kwa kutumia madini ya makaa ya mawe na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) 

Kutokana na shauku hiyo wameiomba STAMICO kuongeza wigo wa usambazaji mkaa mbadala huo ndani na nje ya mipaka ya nchi  ili kuwafikia watumiaji wengi.

Akitoa maoni yake mara baada ya kupata elimu ya umuhimu wa kutumia mkaa mbadala wa mkaa utokanao na miti Bw. Isaac Katogo amesema mkaa huu ni mzuri  na ni sehemu ya kutunza mazingira  na kulinda  vyanzo vya maji.

 Naye, Bw. Emmanuel Kayoka amesema  teknolojia ya mkaa Mbadala imekuja wakati muafaka ambapo  dunia na Taifa vipo katika jitihada ya kuzuia uharibifu wa mazingira  unaotokana na ukataji miti.

"Niwapongeze STAMICO  kwa kuja na Mkaa huu ambao umelenga kuongeza chachu ya kuhamasisha utunzaji wa uoto wa asili (misitu)  na kuhakikisha mazingira yanabaki salama"  alisema Bw. Kayoka

STAMICO  imeendelea  kutumia fursa mbalimbali  kuhamasisha matumizi ya mkaa mbadala  sambamba  na kuongeza uzalishaji  kwa kusimika mitambo mikubwa miwili ya kuzalisha mkaa huo ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals