[Latest Updates]: Serikali yasema wasioendeleza maeneo ya uchimbaji madini ujenzi kufutiwa leseni

Tarehe : July 25, 2018, 5:43 a.m.
left

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo,( pili kulia) akiwa katika chumba cha mizani katika mgodi wa Suma JKT ulioingia ubia na kampuni ya uwekezaji ya Uturuki,kukagua zoezi la upimaji wa uzito kwa magari yanayobeba madini ujenzi kabla ya kutoka mgodini.[/caption]

Serikali imesema itazifutia leseni za umiliki kampuni zote na wamiliki wa ardhi walioomba leseni za uchimbaji madini ya ujenzi ikiwemo mchanga, kokoto pamoja na mawe kwa kushindwa kuendeleza maeneo hayo kwa lengo lililokusudiwa.

Kauli hiyo ilitolewa  na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus  Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua migodi ya uchimbaji wa madini ya ujenzi  yaliyopo katika Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani pamoja na kuzungumza na wakazi wa vijiji hivyo, Julai 24, 2018.

Nyongo alisema, kuna baadhi ya wamiliki wa ardhi na kampuni mbalimbali zilizoomba  leseni za uchimbaji madini ya ujenzi katika maeneo tofauti nchini,miaka mingi iliyopita pasipo kuyaendeleza na hivyo kusababisha maeneo hayo kuwa vichaka na kuwazuia wengine  kuomba leseni  za uchimbaji na kuendeleza maeneo hayo.

Aidha, alitoa onyo na kuwataka  baadhi ya watu wasiowaaminifu kuacha mara moja tabia ya kuwahadaa wawekezaji wanaotaka kuomba leseni katika maneo ya uchimbaji kwa kuwaeleza kuwa wanamiliki leseni za maeneo hayo na kuwataka waingie nao ubia, jambo ambalo si kweli na kwamba tabia  hiyo inachafua dhana halisi ya uwekezaji nchini.

“Kuna mapori na maeneo mengi nchini yanayofaa katika uchimbaji wa madini ya ujenzi, lakini mtu akijitokeza kutaka kufanya kazi katika moja ya maeneo hayo anaalezwa kuwa eneo hilo linamilikiwa na mtu na linaleseni ya uchimbaji, lakini eneo hilo limeendelea kuwa pori au kichaka kwa miaka mingi, hili haikubaliki. Leseni za aina hiyo lazima zifutwe na tutazifuta hivi karibuni”, alisema Nyongo.

Sambamba na hilo, aliwaagiza maafisa madini wote kushirikiana na Serikali za Vijiji husika kukagua maeneo na leseni zote za uchimbaji madini hayo, kubaini zilizohalali na zisizohalali ili ziweze kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria ya madini.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo( katikati) akitembelea Mgodi wa SumaJKT ulioingia ubia na kampuni ya uturuki.

Vilevile, aliwata baadhi ya wamiliki wa migodi ya uchimbaji madini ya mchanga, wenye tabia ya kutorosha madini hayo na kukwepa kulipa mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 na kufanyiwa Marekebisho 2017, kuacha mara moja tabia hiyo na kwamba sheria itachukuwa mkondo wake kwa yeyote atakayebainika.

"Nawaonya wale wote wenye tabia ya kuchimba madini ujenzi, kwa maana ya kokoto, mchanga, mawe kisha kuyatorosha na kukwepa kulipa mrabaha na tozo, pindi utakapokamatwa serikali haitavumilia uhalifu huo kwani unaipoteza mapato,tutakufutia leseni na kutaifisha vifaa vyako vyote", alisisitiza Nyongo.

Hata hivyo, aliwaagiza maafisa madini kuangalia uwezekano wa kubadilisha vocha za ulipaji mrabaha kuwa wa kieletroniki ili kuweka utaratibu mzuri wa ukusanyaji wa maduhuli ya serikali.

Akizungumzia suala la ulipuaji wa miamba, lililolalamikiwa na wananchi, Nyongo aliwashauri wamiliki wa migodi katika maeneo hayo, kuzungumza na wananchi wa maeneo husika ikiwezekana kuwalipa fidia ili wananchi hao waweze kuondoka katika maeneo hayo kuepuka  madhara yanayoweza kutokea.

Pia aliwashauri wananchi hao kuwa, endapo watakubalina na wawekezaji hao, kuridhia kile watakachokubaliana ili kuondoa migogoro na migongano ambayo hutokea mara kwa mara kati ya muwekezaji na wananchi mara baada ya kulipwa fidia ama vinginenyo.

Mwaka 2017, serikali kupitia Wizara ya Madini ilikusanya zaidi ya shilingi bilioni 8, ikiwa ni mrabaha pamoja na tozo mbalimbali zilizotokana na sekta ya madini pekee.

akiwa wilayani bagamoyo, nyongo alitembelea baadhi ya migodi ya uchimbaji madini ya mchanga ukiwepo wa Suma JKT uliyoingia ubia na kampuni ya uwekezaji kutoka nchini Uturuki, mgodi wa kampuni ya Ashraf, Mgodi wa kampuni ya uwekezaji ya Yaate ulioshinda tenda ya kuzalisha kokoto za aina zote zinazotumika katika ujenzi wa reli ya kisasa( Standard Gauge)kutoka Dar es salaam hadi Dodoma, mgodi wa kampuni ya Tan-Turk, mgodi wa kampuni ya uwekezaji Even pamoja na mgodi wa kampuni ya Kerai.

Imeandaliwa na:

Zuena Msuya, Pwani

Afisa Habari,

Wizara ya Madini,

Kikuyu Avenue,

P.O Box 422,

40474 Dodoma,

Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,

BaruaPepe: info@madini.go.tz,                                             

Tovuti: madini.go.tz

 

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals