[Latest Updates]: Nyongo asema Wizara ya Madini haitotoa leseni kwa mwekezaji mbabaishaji wilayani Misungwi

Tarehe : April 28, 2018, 12:06 p.m.
left

Naibu waziri wa Madini,  Stanslaus Nyongo amesema kuwa Wizara yake  haitatoa leseni ya uchimbaji madini kwa mwekezaji aliyepewa leseni ya kuchimba  madini katika  eneo la kijiji cha Ishokelahela  wilaya ya Misungwi baada ya kushindwa kuendeleza eneo hilo kama Sheria ya Madini inavyoelekeza.

Akiwa katika ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wilayani humo,  Nyongo alisema kuwa mwekezaji huyo alipewa leseni ya uchimbaji wa madini kwa kipindi cha miaka 10 na hakuna uendelezaji wowote  alioufanya katika machimbo hayo.

Uamuzi huo umetokana  na malalamiko  ya  wananchi  wa  kijiji  hicho  wakati wakitoa dukuduku zao kwa Waziri Mkuu kuwa, mwekezaji  huyo amekuwa akiwazuia wachimbaji wadogo kuchimba madini katika machimbo hayo hali iliyopelekea Waziri Mkuu kumtaka Naibu Waziri wa Madini kulitolea ufafanuzi suala  hilo.

Akitoa ufafanuzi kuhusu mwekezaji huyo,  Nyongo alisema kuwa  kutokana  na kutoendeleza machimbo hayo mwekezaji huyo amekuwa  haelewani na jamii inayozunguka machimbo hayo na kwamba  hapo  awali  wananchi walikuwa wanafanya shughuli za  uchimbaji katika  katika eneo hilo kabla ya kupewa mwekezaji huyo.

‘’Mwekezaji huyu anayefahamika kwa jina la Badir Soud kwa kuwa leseni yake imeisha na ameomba tena leseni hiyo ya uchimbaji hatutampa, na sisi kama Wizara ya Madini tutawapatia wananchi wachimbe wakiwa katika mfumo wa vikundi’’ alisema Nyongo.

Aliendelea kueleza kuwa,  pamoja na kutokuendeleza mgodi huo katika kipindi hicho,  mwekezaji huyo hajapeleka vifaa kwa ajili ya shughuli za uchimbaji katika eneo la mgodi jambo ambalo linaikosesha Serikali mapato.

Naibu Waziri Nyongo alitumia fursa hiyo kuwaagiza wachimbaji wa madini nchini kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria  za uchimbaji madini  ili waweze kutambulika rasmi na kuweza kulipa kodi serikalini.

Na Mwandidhi Wetu Misungwi

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals