[Latest Updates]: Waziri Kairuki ataka migogoro yote ya madini isuluhishwe ndani ya mwaka mmoja

Tarehe : May 4, 2018, 9:54 a.m.
left

Waziri wa Madini Angellah Kairuki amewataka watendaji wote wa Wizara hiyo kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi na kutatua migogoro yote iliyopo katika sekta husika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.

Viongozi na Wajumbe mbalimbali wakiwa katika ufunguzi wa kikao kazi cha Maafisa Madini wa Kanda, Mikoa na wataalam mbalimbali wa Wizara ya Madini kilichofanyika Mei 3, 2018 Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.[/caption]

Ametoa maagizo hayo mapema leo, Mei 3, 2018 wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Madini wa Kanda, Mikoa na wataalam mbalimbali wa Wizara ya Madini kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.

“Lengo la Wizara ni kuhakikisha migogoro katika sekta ya madini inakwisha kabisa. Nawapongeza Naibu Mawaziri kwa kusimamia zoezi la utatuzi wa migogoro mbalimbali ambapo, mingi imekwishatatuliwa.”

Aidha, Waziri Kairuki amewaagiza watendaji na wataalam hao wa sekta ya madini, kuandaa taarifa fupi za migogoro iliyopo katika maeneo yao zikiainisha aina ya mgogoro, hatua zipi za utatuzi zimechukuliwa hadi sasa pamoja na ushauri wao kuhusu nini kifanyike ili kuhakikisha mgogoro husika unatatuliwa.

Katika hatua nyingine, pamoja na kupongeza ufanisi ulioonekana katika ukusanyaji wa maduhuli, Waziri amewataka watendaji hao kuongeza bidii na ubunifu zaidi ili kuhakikisha wanafanya vizuri zaidi katika eneo hilo.

Amewataka kutekeleza ipasavyo majukumu yao ya kazi, pamoja na kuzingatia umuhimu wa dhana ya ushirikishaji majukumu mahala pa kazi, ili kupata matokeo bora zaidi.

“Kila mmoja aangalie Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano unataka nini na aone jinsi gani anautekeleza katika nafasi yake,” alisisitiza.

Viongozi na Wajumbe mbalimbali wakiwa katika ufunguzi wa kikao kazi cha Maafisa Madini wa Kanda, Mikoa na wataalam mbalimbali wa Wizara ya Madini kilichofanyika Mei 3, 2018 Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.[/caption]

Vilevile, amewataka kuhakikisha wanakuwa na uelewa mzuri wa sheria na kanuni mpya za madini ili waweze kuzitekeleza kikamilifu.

Kuhusu suala la usalama migodini, Waziri kairuki amewataka watendaji kuendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa madini, wananchi wanaozunguka migodi na wadau wengine kwa ujumla kuhusu namna ya kuepusha ajali katika maeneo yao.

Ameshauri na kusisitiza kuwa mafunzo hayo yatolewe kwa kutumia lugha rahisi ili hata wale wenye elimu ndogo waweze kuelewa.

Ufunguzi wa kikao kazi hicho cha siku tatu, umehudhuriwa pia na Naibu Mawaziri wa Madini, Dotto Biteko na Stanslaus Nyongo, Katibu Mkuu wa Wizara husika Prof. Simon Msanjila, Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula, Kamishna wa Madini na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Prof Shukran Manya pamoja na viongozi na wataalam mbalimbali wa Wizara hiyo.

Imeandaliwa na:

Veronica Simba, Dodoma

Afisa Habari,

Wizara ya Madini,

Kikuyu Avenue,

P.O Box 422,

40474 Dodoma,

Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,

BaruaPepe: info@madini.go.tz,                                             

Tovuti: madini.go.tz

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals