[Latest Updates]: Ujenzi wa Mgodi wa mfano Lwamgasa wafikia asilimia 80

Tarehe : Oct. 27, 2018, 8:34 a.m.
left

Na Asteria Muhozya,

Wizara ya Madini imeanza kukutana na Kamati Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuanzia leo tarehe 29 Oktoba hadi Novemba 1, 2018.

Katika kikao cha leo Wizara imewasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

Akiwasilisha Taarifa kuhusu Ujenzi wa Mgodi wa Mfano wa Lwamgasa,  Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Madini, Augustine Ollal amesema hadi kufikia mwezi Septemba,2018, kazi ya ujenzi wa mgodi na usimikaji wa mitambo ya uchenjuaji imekamilika kwa asilimia 80.

Kuhusu mradi wa One Stop Center, eneo la Mirerani, amesema uko kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi  na kuongeza kuwa,   jengo hilo litakapokamilika litakuwa na miundombinu  mbalimbali ikiwemo huduma za Utoaji na Usimamizi wa Leseni za Madini, Uhifadhi wa madini kwa usalama  , Kodi na tozo mbalimbali ikiwemo ofisi za TRA, Huduma za kifedha, ikiwemo Benki na Ofisi za Benki kuu, Huduma za tathmini na uthamini madini, Ofisi za Madini na Chumba maalum cha kufanyia minada ya madini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals