[Latest Updates]: Sekta ya Madini Ndiyo Sekta Mama ya Uchumi wa Tanzania – Dkt. Kiruswa

Tarehe : Nov. 16, 2024, 12:32 p.m.
left

Dondoo za Mahojiano ya Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa katika Kipindi cha Kiss Ripoti - Kiss FM, Novemba 15, 2024

Kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji wa Sekta ya Madini Tanzania 2024

•    Dhima: "Kuongezea Thamani Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii."

•    Malengo ya Mkutano:

•    Kutangaza fursa zilizopo katika sekta ya madini.
•    Kubadilishana uzoefu na kukuza uwekezaji.
•    Kujadili teknolojia za kisasa za uchimbaji na usafishaji madini.
•    Kuhakikisha madini yanachangia katika uchumi kwa kuongezewa thamani.

Nafasi ya Tanzania Katika Sekta ya Madini

•    Tanzania inaendelea na mkakati wa kuwa kitovu cha madini barani Afrika.
•    Nchi nyingine zinajifunza kutoka Tanzania kuhusu usimamizi bora wa sekta ya madini mfano mzuri ni majirani zetu Malawi. 
•    Utafiti wa kina wa madini umeimarishwa, nanSerikali imewekeza zaidi katika miundombinu ya sekta.

Mnyororo wa Sekta ya Madini:

•    Kuanzia utafiti, uchimbaji, usafishaji, biashara, na utoaji wa huduma migodini.

Madini Mkakati:

•    Tumejaaliwa kuwa na aina nyingi za madini muhimu yanayohitajika kwa ajili ya nishati safi kama vile nikeli, kobalti, kinywe, gesi ya Helium na mengine. 
•    Madini muhimu kwa nishati safi ni nyenzo za kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
•    Madini haya yanachangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi huku yakilinda mazingira.
•    Mwekezaji yeyote anayekuja kuwekeza nchini lazima atuonyeshe mpango wa kuyasafisha au kuyaongezea thamani hapa hapa nchini madini muhimu. 

Uwezeshaji:

•    Tozo zimepunguzwa kutoka zaidi ya 30% hadi 9.3%.
•    Wachimbaji wa dhahabu wanaotumia refineries za ndani wamepewa msamaha maalum wa kodi.
•    Benki Kuu ya Tanzania sasa inanunua dhahabu ili kuimarisha akiba ya fedha za kigeni.

Mfumo wa Masoko:

•    Masoko 43 na vituo vya ununuzi wa madini 105 yameanzishwa ili kuhakikisha wachimbaji wanapata uhakika wa soko na bei elekezi.
•    Mfumo huu pia unasaidia kudhibiti utoroshaji wa madini na kuimarisha mapato ya serikali.

Programu ya Mining for Brighter Tomorrow (MBT) inalenga vijana na wanawake kwa kuwapatia:

•    Vifaa vya uchimbaji ili wafanye shughuli zao kwa tija zaidi.
•    Kuwapatia Leseni za uchimbaji ili wafanye shughuli zao bila usumbufu. 
•    Elimu kuhusu teknolojia na upatikanaji wa mikopo nafuu kupitia Taasisi za fedha na mabenki kwa uratibu wa serikali.
•    Serikali kupitia STAMICO imeagiza mitambo ya uchorongaji kwa ajili ya wachimbaji wadogo, mitano ilishawasili na kukabidhiwa wachimbaji wadogo na mengine 10 itawasili hivi karibuni.
•    Msaada wa vifaa maalum, kama magari kwa kina mama.

Mafanikio na Malengo ya Sekta

•    Sekta ya madini inachangia 9% ya Pato la Taifa (GDP), huku lengo likiwa kufikia 10% mwaka 2025.
•    Tanzania ni nchi ya kwanza Afrika kurasimisha sekta ya uchimbaji mdogo, jambo linalosaidia kukuza ajira na uchumi wa jamii.

Ushirikiano wa Sekta ya Madini na Jamii

•    Uchimbaji Mkubwa:
•    Kampuni kubwa zinatekeleza wajibu wa kijamii (CSR) kwa jamii zinazozunguka miradi yao kama vile ujenzi wa miradi kwa ajili ya huduma za kijamii, barabara, maji na kadhalika.

•    Utekelezaji wa Ushiriki wa Watanzania:
•    Mkazo umewekwa katika local content, kuhakikisha Watanzania wanashiriki moja kwa moja katika sekta ya madini kupitia ajira, huduma, na biashara.
•    Hii ni sehemu ya jitihada za serikali kuifanya sekta ya madini kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa watanzania wote.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals