Tarehe : Nov. 16, 2024, 12:32 p.m.
Dondoo za Mahojiano ya Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa katika Kipindi cha Kiss Ripoti - Kiss FM, Novemba 15, 2024
Kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji wa Sekta ya Madini Tanzania 2024
• Dhima: "Kuongezea Thamani Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii."
• Malengo ya Mkutano:
• Kutangaza fursa zilizopo katika sekta ya madini.
• Kubadilishana uzoefu na kukuza uwekezaji.
• Kujadili teknolojia za kisasa za uchimbaji na usafishaji madini.
• Kuhakikisha madini yanachangia katika uchumi kwa kuongezewa thamani.
Nafasi ya Tanzania Katika Sekta ya Madini
• Tanzania inaendelea na mkakati wa kuwa kitovu cha madini barani Afrika.
• Nchi nyingine zinajifunza kutoka Tanzania kuhusu usimamizi bora wa sekta ya madini mfano mzuri ni majirani zetu Malawi.
• Utafiti wa kina wa madini umeimarishwa, nanSerikali imewekeza zaidi katika miundombinu ya sekta.
Mnyororo wa Sekta ya Madini:
• Kuanzia utafiti, uchimbaji, usafishaji, biashara, na utoaji wa huduma migodini.
Madini Mkakati:
• Tumejaaliwa kuwa na aina nyingi za madini muhimu yanayohitajika kwa ajili ya nishati safi kama vile nikeli, kobalti, kinywe, gesi ya Helium na mengine.
• Madini muhimu kwa nishati safi ni nyenzo za kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
• Madini haya yanachangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi huku yakilinda mazingira.
• Mwekezaji yeyote anayekuja kuwekeza nchini lazima atuonyeshe mpango wa kuyasafisha au kuyaongezea thamani hapa hapa nchini madini muhimu.
Uwezeshaji:
• Tozo zimepunguzwa kutoka zaidi ya 30% hadi 9.3%.
• Wachimbaji wa dhahabu wanaotumia refineries za ndani wamepewa msamaha maalum wa kodi.
• Benki Kuu ya Tanzania sasa inanunua dhahabu ili kuimarisha akiba ya fedha za kigeni.
Mfumo wa Masoko:
• Masoko 43 na vituo vya ununuzi wa madini 105 yameanzishwa ili kuhakikisha wachimbaji wanapata uhakika wa soko na bei elekezi.
• Mfumo huu pia unasaidia kudhibiti utoroshaji wa madini na kuimarisha mapato ya serikali.
Programu ya Mining for Brighter Tomorrow (MBT) inalenga vijana na wanawake kwa kuwapatia:
• Vifaa vya uchimbaji ili wafanye shughuli zao kwa tija zaidi.
• Kuwapatia Leseni za uchimbaji ili wafanye shughuli zao bila usumbufu.
• Elimu kuhusu teknolojia na upatikanaji wa mikopo nafuu kupitia Taasisi za fedha na mabenki kwa uratibu wa serikali.
• Serikali kupitia STAMICO imeagiza mitambo ya uchorongaji kwa ajili ya wachimbaji wadogo, mitano ilishawasili na kukabidhiwa wachimbaji wadogo na mengine 10 itawasili hivi karibuni.
• Msaada wa vifaa maalum, kama magari kwa kina mama.
Mafanikio na Malengo ya Sekta
• Sekta ya madini inachangia 9% ya Pato la Taifa (GDP), huku lengo likiwa kufikia 10% mwaka 2025.
• Tanzania ni nchi ya kwanza Afrika kurasimisha sekta ya uchimbaji mdogo, jambo linalosaidia kukuza ajira na uchumi wa jamii.
Ushirikiano wa Sekta ya Madini na Jamii
• Uchimbaji Mkubwa:
• Kampuni kubwa zinatekeleza wajibu wa kijamii (CSR) kwa jamii zinazozunguka miradi yao kama vile ujenzi wa miradi kwa ajili ya huduma za kijamii, barabara, maji na kadhalika.
• Utekelezaji wa Ushiriki wa Watanzania:
• Mkazo umewekwa katika local content, kuhakikisha Watanzania wanashiriki moja kwa moja katika sekta ya madini kupitia ajira, huduma, na biashara.
• Hii ni sehemu ya jitihada za serikali kuifanya sekta ya madini kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa watanzania wote.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.