Tarehe : Aug. 1, 2024, 11:52 a.m.
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amewaongoza Watumishi Wizara ya Madini na baadhi ya taasisi zake kumuaga Mtumishi wa Wizara ya Madini Afisa Hesabu Mwandamizi Humphrey Nyange aliyefariki Dunia Julai 28, 2024 katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma alikokuwa akitibiwa.
Akizungumza leo Agosti Mosi 2024, Nyumbani kwa marehemu Meliwa jijini Dodoma, Waziri Mavunde ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa watumishi na marafiki na kumwelezea marehemu Humphrey kuwa mtu ambaye katika majukumu yake alihakikisha kila aliyestahili kupata haki yake anaipata kwa wakati.
Pia, amemwelezea kuwa ni mtumishi aliyejali wenzake na kutamani kutengeneza furaha kwa wenzake na kusema, “Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya maisha yake, alikuwa ni mtu mwenye upendo, ushirikiano na zawadi kwa wenzake,” amesema Mhe. Mavunde.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.