[Latest Updates]: Wachimbaji madini Kigoma waeleza changamoto zao kwa Naibu Waziri Nyongo

Tarehe : Nov. 1, 2018, 5:07 a.m.
left

Wachimbaji wa Madini wadogo wa Mkoa wa Kigoma, wamemweleza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo changamoto mbalimbali zinazowakabili katika shughuli zao na kumwomba awasaidie kuzitatua.

Kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wachimba Madini Tanzania (FEMATA) Lister Balegele na Msaidizi wa Naibu Waziri, Noel Baraka. Wakati wa Kikao na Wachimbaji Madini wadogo wa Mkoa wa Kigoma, Machi 3 Mwaka huu.[/caption]

Walimweleza changamoto hizo katika kikao maalum, Machi 3 mwaka huu, wakati Naibu Waziri alipowatembelea akiwa katika ziara ya kazi mkoani humo.

Miongoni mwa changamoto kubwa waliyoitaja ni kuhusu vibali vya kusafirisha madini ghafi nje ya nchi; ambapo Naibu Waziri aliwataka kuwa wavumilivu kwani Serikali inakamilisha mchakato wa kuandaa Mwongozo maalum utakaopambanua kila aina ya madini yaliyo nchini na yanapaswa kusafirishwa yakiwa katika hali gani.

“Unajua, Madini yanatofautiana, na uchakataji wake unatofautiana. Hivyo tumeona tuandae Mwongozo utakaoondoa mkanganyiko huo na kuwarahisishia kujua Madini gani yanapaswa kuongezewa thamani kwa kiwango kipi ili uruhusiwe kuyasafirisha nje ya nchi.”

Alisema kuwa, Mwongozo huo utatolewa hivi karibuni na hivyo Serikali itaanza tena kutoa vibali vya usafirishaji Madini nje ya nchi.

Vilevile, wachimbaji hao walitaja changamoto nyingine kuwa ni upatikanaji wa Ruzuku ambapo pamoja na kulalamikia Serikali kusimamisha zoezi hilo, lakini pia walidai kuwa wakati ikitolewa, wahusika hawakutenda haki.

“Wasiokuwa na vigezo ndiyo walikuwa wakipatiwa Ruzuku ilhali wenye vigezo wakinyimwa,” walilalamika.

Akizungumzia suala hilo, Naibu Waziri aliwaeleza kuwa Serikali iliamua kusimamisha kwa muda zoezi la utoaji Ruzuku kutokana na kugundua udhaifu katika zoezi husika ikiwemo baadhi ya wanufaika kutumia Ruzuku waliyopewa kwa mambo yao binafsi tofauti na masharti yake. Hata hivyo, alisema kuwa Ruzuku itaanza kutolewa tena baada ya Serikali kujiridhisha kuwa itatumika vema.

Kuhusu suala la wenye vigezo kunyimwa Ruzuku na wasio na vigezo kupatiwa; Naibu Waziri alisema Serikali itafuatilia na kuchunguza kwa ukaribu ili kuwabaini watumishi wa umma na wengine wanaoshirikiana nao katika kupindisha utaratibu uliowekwa kwa sababu wanaozijua wao.

Baadhi ya Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoa wa Kigoma, wakiwasilisha maoni yao kwa Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo (hayupo pichani), wakati alipowatembelea na kuzungumza nao, akiwa katika ziara ya kazi mkoani Kigoma, Machi 3 Mwaka huu.[/caption]

“Tukiwabaini tutawachukulia hatua kali za kisheria. Nanyi tunawaomba mtuletee aina yoyote ya ushahidi unaoweza kutusaidia kuthibitisha madai yenu ili kwa pamoja tukomeshe tatizo hilo.”

Aliongeza kuwa, katika kushughulikia tatizo hilo, tayari Serikali ilishatoa tamko kuwataka wale waliotumia Ruzuku kwa matumizi binafsi tofauti na masharti yake, wazirudishe pesa hizo mara moja na kwamba muda waliopewa kurudisha umekwisha, hivyo wataanza kushughulikiwa.

Wachimbaji hao pia walilalamikia kutopewa ushirikiano na watumishi wa Ofisi ya Madini Kigoma ambapo Naibu Waziri aliahidi kufuatilia na kushughulikia suala hilo.

Imeandaliwa na:

Veronica Simba, Kigoma

Afisa Habari,

Wizara ya Madini,

Kikuyu Avenue,

P.O Box 422,

40474 Dodoma,

Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,

BaruaPepe: info@madini.go.tz,                                             

Tovuti: madini.go.tz

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals