Tarehe : March 28, 2018, 9:09 a.m.
Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wamekutana Jijini Arusha ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu madini hayo kwa maslahi mapana ya nchi hizo.
Mwenyekiti wa mkutano, Service Julie kutoka Congo (wa pili kulia) akizungumza wakati wa Mkutano wa Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR.[/caption]
Mkutano huo wa siku mbili ulifunguliwa jana Machi 27, 2018 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ambapo alisisitiza kuwa Nchi Wanachama wa ICGLR wanao wajibu wa pamoja kuhakikisha malengo waliyojiwekea yanafikiwa kwa manufaa ya wanachama wote.
Gambo alizungumzia changamoto mbalimbali zinazozikabili Nchi Wanachama ambazo ni uvunaji haramu wa madini, utoroshwaji wa madini, uharibifu wa mazingira, ukosefu wa teknolojia na baadhi ya Nchi kuwa na changamoto za Kiusalama.
Hata hivyo alisema changamoto hizo zisiwe sababu ya kurudi nyuma badala yake juhudi za pamoja, mshikamano wa dhati unahitajika ili kukabiliana na changamoto hizo na kuhakikisha ufumbuzi unapatikana kwa maslahi mapana ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.
Nchi Wanachama ni Tanzania, Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Congo (Kinshasa), Congo (Brazzaville), Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Sudan Kaskazini, Uganda na Zambia.
Tanzania imekuwa Mwanachama rasmi wa ICGLR Mwaka 2008 na tangu wakati huo imeendelea kutekeleza malengo ya mpango wa ICGLR ili kufanikisha udhibiti wa uvunaji haramu wa madini na kuhakikisha manufaa ya pamoja ya rasilimali husika yanapatikana.
Imeandaliwa na:
Mohamed Saif,
Afisa Habari,
Wizara ya Madini,
5 Barabara ya Samora Machel,
S.L.P 2000,
11474 Dar es Salaam,
Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,
Barua Pepe: info@madini.go.tz,
Tovuti: madini.go.tz
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.