[Latest Updates]: Sera ya Kuongeza Thamani Madini Mkakati Yashika Kasi Afrika

Tarehe : Oct. 18, 2023, 8:30 a.m.
left

#Dkt. Kiruswa kutangaza fursa za Madini Muhimu yaliyopo nchini

Naibu Waziri wa Madini, Dkt Steven Kiruswa Oktoba 17, 2023 aliongoza ujumbe    wa Tanzania katika ufunguzi wa Mkutano wa Madini Muhimu na Mkakati  kwa mwaka 2023 unaofanyika katika Jiji la Cape Town nchini Afrika Kusini.

Mkutano huo unahudhuriwa na Viongozi, Watalaam, Taasisi za Fedha, Watengenezaji wa  vifaa vya kielektroniki na baadhi ya Wawaziri wa Nchi za Afrika  ikiwemo Msumbiji, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zimbabwe, Malawi, Tanzania na Sudan Kusini.

Aidha, leo Oktoba 18, 2023, Mkutano huo utaendelea ambapo Tanzania kupitia  Naibu Waziri Dkt. Kiruswa ataeleza kuhusu fursa za Madini Muhimu na Mkakati  zilizopo nchini  pamoja  na Sera ya ujenzi wa mitambo ya kuchakata madini hayo ndani ya nchi.

Katika mkutano huo, Dkt. Kiruswa ameambatana na watalaam kutoka wizarani ambao ni; Kamishna Msaidizi wa Madini Mhandisi  Ally Samaje, Mkurugenzi wa Huduma za Maabara kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti Wa Madini Tanzania (GST) - Notka Banteze pamoja na Mjiolojia  Joseph Ngulumwa.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals