[Latest Updates]: Waziri Mavunde Atoa Onyo Watoroshaji Madini Nchini

Tarehe : Oct. 19, 2023, 8:34 a.m.
left

# Utoroshaji Madini kunaikosesha Serikali Mapato

# Aeleza zaidi ya Kilogram 4 za madini zilikamatwa Kahama


Serikali imewataka wadau wote wa sekta ya Madini nchini kutojihusisha na vitendo vya  utoroshaji madini katika maeneo yoyote yenye uchimbaji, uhifadhi na Uuzaji kwani kwa kufanya hivyo kunaikosesha Serikali kupata mapato yatokanayo na rasilimali madini.

Hayo yamebainishwa leo tarehe Oktoba 19 , 2023 na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde wakati akizungumza na Wanachama wa Chama cha Mabroka Tanzania (CHAMMATA) jijini Dodoma.

Mhe.Mavunde amesema kuwa Serikali ina mipango mingi  katika kuendeleza sekta ya Madini lengo ikiwa ifikapo mwaka 2025 sekta hii kuchangia asilimia zaidi y kumi (10%) katika pato la Taifa (GDP) kama mpango wa Maendeleo wa Dira  ya Taifa 2025 unavyoelekeza.

Akielezea kuhusu mchango wa Madini katika Pato laTaifa Mhe.Mavunde alifafanua kuwa katika Mwaka 2022/2023 sekta ya Madini ilikusanya zaidi ya bilioni Mia sita huku asilimia 40 ikichangiwa na wachimbaji wadogo , wafanyabiashara wa madini wa ndani na Broka.

Akielezea kuhusu mzunguko wa fedha katika mnyororo mzima wa sekta ya madini , Mhe.Mavude amesema kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) iliweza kukusanya mapato ya kodi ya ndani kiasi cha Trilioni mbili hii ni kulingana na mzunguko wa pesa katika masoko ya ndani ya madini.

Naye , Mwenyekiti wa chama cha  CHAMMATA Jeremia Kituyo ameshauri kuwa ili kuondokana na utoroshaji wa madini nchini ni vyema Serikali ikaja na mpango wa kukate  leseni kwa mfumo wa kikanda hiyo itatoa wigo mpana kwa wafanyabiashara kutoka kanda moja na nyingine.

Kituyo aliongeza kuwa ni muda muafaka sasa serikali ikaiweka  biashara ya madini kuwa biashara huria katika masoko ya madini hususani katika minada hii itawezesha bei kuwa shindani katika masoko ya madini.

Akielezea kuhusu lengo la kuanzishwa  kwa CHAMMATA Kituyo alifafanua kuwa lengo ni kuwaunganisha wafanyabiashara wa madini na Serikali pamoja na  kutetea na kusimamia haki za wafanyabiashara wa madini nchini.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals