[Latest News]: Waziri Biteko Asisitiza Miradi Yenye Madini Mkakati Kuendelezwa

Tarehe : July 21, 2022, 9:58 p.m.
left

Serikali imetoa agizo kwa wawekezaji katika Sekta ya Madini kuendeleza maeneo yao yenye madini ya kimkakati badala ya kuyaacha bila kuyaendeleza suala linalopelekea wenye nia ya kuwekeza kukosa fursa hiyo.

Amesema wapo wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika Sekta hiyo maeneo mbalimbali nchini lakini wanashindwa sababu baadhi yao wanakaa na maeneo kwa muda mrefu bila kuyaendeleza.

Hayo yamebainishwa Julai 21, 2022 na Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko katika kijiji cha Mgambazi wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma alipotembelea Kampuni ya Lubalisi Resources Ltd inayofanya utafiti wa madini ya Nikeli.

Amewasisitiza wawekezaji katika Sekta ya Madini wanapaswa kufuata Sheria na Taratibu zilizowekwa katika uwekezaji huo ili kuepuka kufutiwa leseni zao.

Aidha, amewataka wawekezaji hao kuwasilisha taarifa za kipindi cha miezi mitatu ya utekelezaji kazi ya utafiti wa madini iliyofanyika kwa kipindi husika (quarterly report) ambayo husaidia kujua mwenendo au maendeleo ya mradi ya utafiti wa madini.

Amesema lengo la taarifa hizo ni kuiwezesha Serikali kutambua maendeleo ya mradi kwa kipindi husika.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Hanafi Msabaha amewataka wawekezaji kuchangia katika huduma mbalimbali za kijamii ili jamii zinufaike na uwepo wa madini. Amesema ushirikishwaji wa wananchi utasaidia kupunguza malalamiko yanayojitokeza mara kwa mara kuhusu wawekezaji.

Naye, Mratibu wa Mradi na Mawasiliano ya Jamii Ashery Lemelo amemuakikishia Dkt. Biteko kusimamia maelekezo yaliyotolewa na Serikali katika mradi huo.

Katika wilaya ya Uvinza tafiti zinaonesha kuwa na madini ya Nikeli. Madini hayo hutumika katika utengenezaji wa bidhaa za magari ya umeme ikiwemo betri na vifaa mbalimbali vya umeme. Aidha, madini ya mkakati yenye uhitaji mkubwa nchini ni pamoja na madini ya Kinywe.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals