Tarehe : March 28, 2018, 9:05 a.m.
Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko amesema Ujenzi wa Ukuta kuzunguka Migodi ya Mirerani ni jambo la Kihistoria na kwamba linatarajiwa kuweka rekodi Barani Afrika.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Issa Nchasi, (wa pili kulia) wakibadilishana jambo na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi wa Ukuta wa Mirerani.[/caption]
Naibu Waziri Biteko aliyasema hayo tarehe 23 Machi, wakati wa kikao cha Maandalizi ya Uzinduzi wa Ukuta huo unaotarajiwa kuzinduliwa mapema mwezi Aprili na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.
Aliongeza kuwa, ukuta huo ni jambo ambalo watanzania wamelisubiri kwa miaka mingi licha ya kuwepo kwa mapendekezo na sasa hatua zimechukuliwa na kutekelezwa.
Pia alilipongeza Jeshi kwa nidhamu kubwa ambayo limeonesha kwa ujenzi wa ukuta huo wenye urefu wa kilomita 25.4 na ambao ujenzi wake umechukua kipindi cha miezi 3 tofauti na ilivyopangwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti, alilipongeza Jeshi kwa kazi ambayo imefanyika na kuwataka Wajumbe wa Kamati kukamilisha utekelezaji wa majukumu yote kwa wakati.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti, Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Zephania Chaula, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Manyara na Wilaya ya Simanjiro, Wizara ya Madini, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ ) Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) , Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO - Manyara) na Wakala wa Barabara ( TANROAD)
Imeandaliwa na:
Asteria Muhozya, Mirerani
Afisa Habari,
Wizara ya Madini,
5 Barabara ya Samora Machel,
S.L.P 2000,
11474 Dar es Salaam,
Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,
Barua Pepe: info@madini.go.tz,
Tovuti: madini.go.tz
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.