[Latest Updates]: Vision 2030 Kugusa Maisha ya Kila Mtanzania wa Kawaida - Mahimbali

Tarehe : Nov. 6, 2023, 4:39 p.m.
left

Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Kheri Mahimbali amesema kuwa dhumuni au dhana kubwa ya 'Vision 2030' ni kuhakikisha kila Mtanzania wa kawaida anajua ni kwa namna gani Sekta ya Madini inamgusa kwenye maisha yake.

Amesema hayo leo Novemba 06, 2023, jijini Dodoma, wakati akizungumza katika kipindi cha runinga na radio cha Good Morning kinachorushwa na Wasafi Media.

“Vision 2030 inalenga kuleta mageuzi makubwa katika Sekta ya Madini kwa kuboresha maisha ya Watanzania wa kawaida, uchumi kwa ujumla sambamba na kufungamanisha sekta zingine tunataka wananchi wanufaike na uwepo wa rasilimali hii.” amesema Mahimbali.

Amesema kuwa kupitia utafiti wa kina wa jiosayansi kutakuwa na kanzidata ya kutosha kuhusu miamba yote yenye madini, maji pamoja na aina ya udongo kwa sehemu husika, hapo tayari sekta ya madini imefungamanisha sekta ya kilimo na maji, na kwamba sekta hizo huwagusa Watanzania katika kawaida.

Akizungumzia Wachimbaji Wadogo, Mahimbali amesema taarifa hizo za zitasaidia wachimbaji hao wachimbe sehemu zenye uhakika na kupelekea kupunguza hatari ya kupoteza fedha na mitaji yao kwa kufanya kazi bila kubahatisha.

Katika hatua nyingine, Mahimbali amesema kupitia Vision 2030, ushirikishwaji wa Watanzania utaimarika katika mnyororo mzima wa Sekta ya Madini na kwamba kufikia 2030

Kwa upande wa Wajibu wa Kampuni kwa Jamii, Mahimbali amesema Serikali kupitia Wizara ya Madini inatatua kero za huduma za kijamii katika maeneo uchimbaji unapofanyika.

“Maeneo ambayo shughuli za uchimbaji zinafanyika tutaenda kutatua kero za wananchi wa pale kwa kuwajengea shule, vituo vya afya, barabara na miundombinu yote muhimu ili kuboresha mazingira yao, lakini sio wizara itaamua bali ni halmashauri zao kwa kuangalia vipaumbele walivyojiwekewea.” amesema Mahimbali.

Kwa upande wake, Kamishna wa Madini kutoka Wizara ya Madini, Dkt. Abdul Rahman Mwanga amesema kuwa hakuna sehemu mashimo yatakapoachwa baada ya shughuli za uchimbaji kukamilika kwa kuwa masharti ya leseni yanaitaka Kampuni zilizowekeza katika sekta ya madini kuwajibika katika kuacha mazingira salama kwa kuwasilisha mpango wa kufunga mgodi Serikalini na kupitishwa baada ya kuridhishwa na mpango huo.

*Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri*

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals