[Latest Updates]: Japan Yaomba Ushirikiano na Tanzania Kuendeleza Madini Mkakati

Tarehe : Feb. 13, 2024, 8:15 a.m.
left

Zaidi ya Wataalam 6 wa GST  Wanufaika  na Mafunzo ya Utafiti wa  Visawe Mbali

Cape Town

Wataalam kutoka Taasisi ya Japan Organisation for Metals and Energy Security (JOGMEC) inayojishughulisha na Utoaji Mafunzo ya Utafiti wa Madini kwa kutumia njia ya Visawe Mbali (Remote Sensing Technology) ya nchini Japan hivi karibuni ilionesha nia ya kushirikiana na Tanzania kuziwezesha kampuni za nchi hiyo zinazojishughulisha na utafiti wa Madini Mkakati nchini.

Hayo yalijiri wakati Tanzania ikishiriki katika Mkutano wa Mining Indaba uliofanyika nchini Afrika Kusini kuanzia tarehe 5 hadi 8 Februari, 2024 ambapo Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa ulipata wasaa wa kukutana na wadau mbalimbali wenye nia ya kuwekeza na kupata taarifa za kina kwenye fursa walizolenga kuwekeza katika Sekta ya Madini nchini.

Katika kikao hicho, JOGMEC ilieleza maeneo ya ushirikiano kwa kampuni za Japan kuwa ni uendelezaji wa madini mkakati ikiwemo copper, nickel, lithium, colbat na manganese ambayo nchi ya Japan ina mahitaji makubwa ya madini hayo. Kutokana na mahitaji makubwa ya madini hayo duniani kuongezeka, inaelezwa kuwa, ifikapo mwaka 2050 mahitaji yake yatafikia tani milioni 150.

Katika Mkutano wa Indaba Tanzania iliweka vipaumbele kutangaza fursa za uwekezaji katika maeneo ya utafiti, utoaji huduma migodini, uchimbaji madini na uongezaji thamani madini ambapo ilitumia mktano maalum wa Tanzania kutangaza fursa zake, midahalo, vikao vya ana kwa ana na maonesho kutangaza uwepo wa fursa za kiuwekezaji katika sekta ya madini kupitia maeneo husika.

Katika kikao hicho, Dkt. Kiruswa aliueleza ujumbe huo kuhusu utayari wa Tanzania kushirikiana na kampuni hiyo kupitia kupitia taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST).

 "Tuko tayari kuwapokea na kufanya makubaliano kupitia taasisi yetu ya GST,’’ alisema Dkt. Kiruswa.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba alisema kuwa, kumekuwepo mahusiano ya muda mrefu na taasisi hiyo kupitia mafunzo ya utafiti wa madini kwa kutumia teknolojia ya visawe mbali ambapo zaidi ya watalaam sita (6) tayari wamenufaika na program ya mafunzo kutoka JOGMEC.

Mwaka 2024, Tanzania imeshiriki kwa Pamoja katika Mkutano wa Mining Indaba kwa kushirikiana na Sekta binafsi chini ya mwanvuli wa Chemba ya Migodi Tanzania ambapo zaidi ya washiriki 100 kutoka Tanzania walishiriki katika mkutano huo mkubwa unaofanyika kila mwaka nchini humo.
 #TANZANIA@The Mining Indaba2024 #InvestInTanzaniaMiningSector

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals