[Latest Updates]: STAMICO Yatwaa Tuzo ya Kujali Jamii

Tarehe : March 1, 2025, 2:02 p.m.
left

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limetwaa Tuzo ya Kujali Jamii (CSR for Women Empowerment)  katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Februari,2025.

Tuzo hiyo iliyokabidhiwa na Mgeni Rasmi, Mhe. Doto Mashaka Biteko, Naibu Waziri Nkuu na Waziri wa Nishati, imeitambua STAMICO kama kinara wa kuwezesha wanawake katika sekta ya madini nchini.

Tuzo hiyo ilipokelewa na Mkurugenzi wa STAMICO wa Rasilimali Watu,Bw Deusdedith Magalla kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji,Dkt Venance Mwasse.

STAMICO ilitajwa kuwezesha wanawake kwa kuwapa uwakala wa nishati ya kupikia ya Rafiki Briquettes vikundi 16 vya Wanawake na Samia.

Pia Shirika limevipatia vikundi sita kontena za futi 40 ili kurahisisha kusambaza nishati hii nchini kote.

Vikundi hivyo ni kutoka mikoa ya Geita,Dodoma,Mbeya,Iringa,Songwe,Ruvuma na Njombe.

Shirika pia limeipatia taasisi ya Foundation for Disabilities Hope (FDH) iliyopo Dodoma inayohudumia watu wenye ualbino kontena la futi 40 pamoja na uwakala wa kusambaza nishati hiyo.

Katika azma yake ya kujali mazingira,STAMICO imeshirikiana na vikundi vya Wanawake na Samia maeneo mbalimbali Tanzania Bara na Visiwani kupanda miti.

Tuzo hiyo ni sehemu ya maandalizi ya Siku ya Kimataifa Duniani (PreIWD) inayoadhimishwa tarehe 8 Machi.

Tanzania itaadhimisha siku hii kitaifa jijini Arusha.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals