[Latest Updates]: Mikoa Mitano Yafaidika na Mitambo ya Kuchoronga Miamba Awamu ya Kwanza

Tarehe : Feb. 12, 2024, 8:13 a.m.
left

● Ina uwezo wa kuchoronga miamba mpaka mita 400

●Lengo ni kuwa na mitambo 15 ifikapo Juni 2024

●Ulinganifu wa gharama za uchorongaji zinazotozwa ni asilimia 47.46 ambazo ni gharama za chini.

Na.Samwel Mtuwa - MoM

Mnamo Oktoba 21,2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alizindua mitambo mitano ya uchorongaji wa miamba aina ya Diamond Core Drilling (DD) ambayo ina uwezo wa kuchoronga miamba kwa mita 400 kuelekea chini ya ardhi.

Mitambo hiyo inayomilikiwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)  yenye lengo la kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini kuweza kuchimba kwa uhakika bila kupoteza mitaji na muda.

Akizungumza katika semina kwa  Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, iliyotolewa hivi karibuni, Mkurugenzi Mkuu wa  STAMICO Dkt. Venance Mwasse alisema kuwa mpango wa  Serikali ni kuwa na mitambo 15 ambayo itasambazwa katika sehemu za wachimbaji wadogo wa madini.

Aliyataja maeneo hayo ambayo ni  Lwamgasa-Geita tayari mita 207 zimechorongwa, Itumbi- Chunya mita 150  Nyamongo -Tarime  mita 153 , na Nhori - Dodoma mita 160 .

Akielezea kuhusu gharama za uchorongaji Dkt.Venance  alifafanua kuwa gharama ya kuchoronga mita moja ni shilingi 227,587.50 ambayo sawa na dola 89.25.

Naye, Meneja wa uchimbaji mdogo kutoka STAMICO Tuna Bandom  alifafanua kuwa  kuhusu ulinganifu  wa gharama za uchorongaji zinazotumika kwa mitambo ya wachimbaji wadogo kwa shimo moja lenye urefu wa mita mia (100m) unagharimu kiasi cha shilingi 108,012.52 ambazo ni sawa na dola za Marekani 42.36.

Bandoma aliongeza kuwa pamoja na gharama ndogo za uchorongaji zinazotozwa kwa wachimbaji wadogo pia wanapata huduma ya bure ya ushauri elekezi  kutoka kwa wataalam wa jiolojia kuhusiana miamba inayochorongwa.

#Vision2030:MadiniNiMaishaNaUtajiri

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals