[Latest Updates]: Rais Magufuli Ampa Tano Waziri Biteko

Tarehe : Nov. 23, 2019, 8:02 a.m.
left

Na Tito Mselem Bukombe,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe Magufuli amempongeza Waziri wa Madini ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe kwa kazi nzuri za maendeleo anazozifanya katika kuleta maendeleo jimboni humo.

Kauli hiyo aliitoa alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi akielekea mapumzikoni Wilayani Chato ambapo alisimamisha msafala wake ili awasalimie wananchi wa Jimbo la Bukombe.

Rais Magufuli amesema anawashukuru sana wananchi wa Bukombe kwa kumchagua Mbunge wa Jimbo hilo ambapo ameeleza kuwa anamsaidia sana katika kutekeleza majukumu yake.

Aidha, Rais Magufuli amewataka wananchi wa Bukombe kuendelea kushirikiana na viongozi wa eneo hilo ambapo amesema amemchagua Biteko kuwa Waziri wa Madini ili atatue migogoro iliyodumu kwa muda mrefu.

“Naomba nichukua fursa hii kuwashukuru sana wananchi wa Bukombe kwa kunichagulia Mbunge huyu, maana ananisaidia sana katika kutimiza majukumu yangu, nawapongeza sana,” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameeleza kwamba, amemchagua Waziri Biteko kwenye Wizara ambayo inachangamoto nyingi katika ukusanyaji wa mapato ambapo kwasasa anaona muelekeo mzuri katika sekta hiyo. 

Wakati huo huo, Rais Magufuli, amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchi kuto kopa mikopo Bank ili wafanye miradi ya maendeleo, kwayeyote atakaye kopa ajiandae kuondoka madarakani.

Kwa upande wake Mbunge wa Bukombe ambae pia ni Waziri wa Madini Doto Biteko amempongeza Rais Magufuli kwa mradi wa Barabara ambapo Rais Magufuli ameongeza mtandao huo kutoka kilometa 256 za lami mpaka kufikia kilometa 1480 na miradi tisa mikubwa ya maji aliyotekelezwa na Rais wa awamu ya tano.

Pia, Waziri Biteko amemshukuru Rais Magufuli kwa kuwapa wananchi eneo la kulima na kuchungia mifago yao ambapo sehemu hizo zilikuwa hifadhi ya taifa.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Biteko amemuomba Rais Magufuli kuangalia uwezekano wa kuongeza mtandao wa barabara kutoka Ushirombo mpaka Katoro

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals