Tarehe : April 28, 2018, 12:03 p.m.
Wizara ya Madini inapenda kuutarifu umma kuwa, tarehe 2 hadi 9 Februari, 2018, Mnada wa Tatu (3) wa mauzo ya almasi kutoka Mgodi wa Mwadui unaomilikiwa na Kampuni ya Williamson Diamonds Limited ulifanyika mjini Antwerp, nchini Ubelgiji.
Katika mnada huo, jumla ya Karati 54,094.47 ziliuzwa kwa thamani ya Dola za Marekani 13,607,858.72 sawa na shilingi 30.6 Bilioni ambapo jumla ya kampuni 145 zilishiriki katika mnada na kuwasilisha zabuni zao za ununuzi na zabuni 1,019 ziliwasilishwa katika mnada huo.
Kufuatia mauzo ya almasi hizo, Serikali imepata Mrabaha wa (Final Royalty) Dola la Marekani 816,471.52 pamoja na Ada ya ukaguzi (Clearance and Inspection) kiasi cha Dola za Marekani 136,078.59 sawa na shilingi za Kitanzania 2,090,164,095.
Aidha, Mrabaha wa awali (Provisional Royalty) uliolipwa kutokana na uthaminishaji wa awali kabla ya mauzo ni Dola za Marekani 674,941.78, ada ya Clearance na Inspection Dola za Marekani 112,490.30 pamoja na Dola za Marekani 100 kwa ajili ya kibali cha kusafirishia almasi ambapo jumla yake ni Dola za Marekani 787,532.08 sawa na shilingi 1,771,947,000.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.