[Latest Updates]: Wizara Tatu Zajadili Hali ya Uzalishaji Chumvi Nchini

Tarehe : Aug. 15, 2024, 6:04 p.m.
left

DODOMA

Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Wizara ya Mipango na Uwekezaji pamoja  na Wizara ya Viwanda na Biashara  zimekutana kujadili namna ya kuondoa changamoto katika sekta ndogo ya chumvi nchini.

Wizara hizo zimekutana leo Agosti 15 , 2024 jijini Dodoma kufuatia  taarifa zilizowasilishwa kwa Serikali na Chama cha Wazalishaji Chumvi Tanzania (TASPA) kuhusu changamoto zinazoikabili sekta hiyo ndogo ya chumvi ikiwemo kudorora kwa biashara ya chumvi hapa nchini.

Kikao hicho kilijumuisha Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Jaffo ,Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Mh. Prof. Kitila Mkumbo na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde pamoja na Wadau wa Chumvi Nchini.

Pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa,Wizara ya Madini kupitia STAMICO imewahakikishia wadau juu ya ufungwaji wa kiwanda cha kusindika Chumvi katika Wilaya ya Kilwa,Mkoa wa Lindi kabla ya
Mwisho wa Mwezi Desemba 2024.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals