[Latest Updates]: Ujenzi wa ukuta umefanyika kwa ubora-Meja Jenerali Busungu

Tarehe : April 9, 2018, 9:18 a.m.
left

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Martin Busungu amesema kuwa ujenzi wa ukuta  unaozunguka Migodi ya Tanzanite Mirerani wenye urefu wa kilomita 24.5, umefanyika kwa ubora na viwango vya juu.

"Vijana wamefanya kazi kwa uzalendo wa hali ya juu na kujitolea. Tumetekeleza kwa ukamilifu weledi na chini ya muda uliopangwa," alisisitiza Meja Jenerali Busungu.

Meja Jenerali Busungu aliyasema hayo wakati wa sherehe za uzinduzi wa ukuta huo uliofanyika tarehe 6 Aprili, 2018, eneo la geti la kuingilia ukuta huo Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara na kuongeza kuwa, ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 5.645,843,163.55.

Meja Jenerali Busungu aliongeza kuwa, matokeo ya ujenzi huo kuwa na ubora na kuchukua kipindi kifupi yalitokana na uadilifu mkubwa wa jeshi na hilo linaonesha kuwa, kazi ya Jeshi si  tu kulinda mipaka, Katiba ya nchi  bali pia kujenga nchi ya Tanzania na kuhakikisha kuwa, rasilimali za zinakuwa salama kwa vizazi vijavyo.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi na wenyeji wa mji wa Mirerani kwa kutoa historia ya eneo hilo ikiwemo mapitio ya maji na njia za wanyama jambo ambalo liliwezesha jeshi hilo kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Pia, alisema kuwa, ukuta huo ulijengwa na vikosi 20 vya jeshi vikijumuisha wataalam wa ujenzi, Wahandisi, Vijana wa JKT wa Operesheni Kikwete na Operesheni Magufuli na Watumishi wa umma.

Imeandaliwa na:

Asteria Muhozya,

Afisa Habari,

Wizara ya Madini,

5 Barabara ya Samora Machel,

S.L.P 2000,

11474 Dar es Salaam,

Simu: +255-22-2121606/7, Nukushi: +255-22-2121606,

Barua Pepe: info@madini.go.tz,                                                                               

Tovuti: madini.go.tz

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals