[Latest Updates]: Dkt. Biteko Aitaka Jamii Inayozunguka Migodi kuwa na Mahusiano Bora na Wawekezaji

Tarehe : July 22, 2022, 10:10 p.m.
left

Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko amezitaka jamii zinazonguka maeneo ya migodi kutangaza mazuri yanayofanywa na wawekezaji katika Sekta ya Madini ili kuwatia moyo wa kufanya shughuli za madini.

Dkt. Biteko ameyabainisha hayo, Julai 22, 2022 akiwa katika ziara yake kijiji cha Kagerankanda wilaya ya Kasulu alipotembelea mgodi wa Kampuni ya Life Business unaochimba madini ya Chokaa mkoani Kigoma.

Amesema, migogoro baina ya wawekezaji katika Sekta ya Madini na wananchi katika maeneo mengi ya migodi imewafanya wawekezaji kupata hofu ya kuwekeza katika uchimbaji wa madini katika baadhi ya maeneo na hivyo kupunguza uzalishaji.

Amewataka wananchi kuhakikisha wanajenga mahusiano mazuri na wawekezaji ili kutatua changamoto zinazojitokeza kati yao ili wawekezaji waweze kutekeleza huduma mbalimbali za kijamii katika maeneo yanayozunguka migodi.

Aidha, Dkt. Biteko ameahidi kuwa, changamoto zilizopo za ukosefu wa barabara na ujenzi wa madarasa zitafanyiwa kazi haraka baada ya kutoa maelekezo kwa mwekezaji huyo.

Kwa upande wake, mmiliki wa mgodi huo ndugu Lister Balegele ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA) amesema, Kampuni hiyo imekuwa ikilipa mapato ya Serikali na michango mbalimbali kutokana na mauzo ya madini ya chokaa.

Kuhusu huduma za kijamii Balegele amesema, mgodi unajenga madarasa mawili mpaka sasa katika shule ya sekondari hapo kijijini, wametoa madawati 50 kwa ajili ya shule pamoja na kugawa kompyuta mpya kwa shule ya sekondari na msingi.

Baada ya ziara ya Dkt. Biteko katika mgodi huo, mwekezaji wa mgodi huo ameahidi kukamilisha barabara na ujenzi wa madarasa hivi karibuni.

Naye, Mjiolojia Mwandamizi kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) John Kalimenze amesema, Serikali kupitia taasisi hiyo itaendelea kufanya tafiti za madini ili iweze kugundua maeneo zaidi kwa ajili ya uchimbaji na kuongeza tija kwa wachimbaji na kuongeza mapato ya Serikali. 

Aidha, amemuhakikishia mwekezaji kupata ushirikiano wa kitaalamu toka GST katika kuendeleza mgodi wake kwa kutambua ubora na wingi wa mashapo ya malighafi ya mawe ya chokaa yaliyopo katika leseni au eneo lake.

Mgodi huo kwa sasa unachimba madini ya chokaa na kusafirisha yakiwa ghafi na kuuza katika kiwanda cha Burundi Cement Company (BUCECO) kupitia mpaka wa Manyovu.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals