[Latest Updates]: Uwekezaji Mkubwa wa Mradi wa Makaa ya Mawe Kiwira

Tarehe : March 9, 2025, 3:18 p.m.
left

ILEJE - SONGWE
Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC)  wakiongozwa na Makamu Mwenyekitii   Ndugu Japhet Hasunga  walifanya ziara kwenye mradi  wa  makaa ya mawe wa Kiwira  ambapo kamati ilitembelea maeneo mbalimbali ya mgodi  ikiwemo  mradi wa kutengeneza nishati mbadala  ya Rafiki Briquette.

Katika ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Deusdedith Magala aliwaongoza wajumbe wa kamati kushudia shughuli  mbalimbali zinazofanywa mgodini hapo zikiwemo 
Uchimbaji na uchakataji wa makaa ya mawe na  mradi wa Rafiki Briquette

Aidha Wajumbe wa Kamati  walipongeza mageuzi na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Shirika katika mgodi wa Kiwira .Wajumbe  pia waliridhishwa na maendeleo ya mradi wa nishati safi ya kupikia ya Rafiki Briquette  na kusisitiza nishati hiyo  muhimu iweze kuwafikia  wananchi wengi  ili kuendelee kuunga mkono ajenda ya  upatikanaji wa Nishati safi kwa Watanzania 

Aidha mheshimiwa Naibu Waziri wa Madini Dkt Steven Kiruswa  ambae aliambatana na Kamati katika ziara hiyo aliishukuru kamati kwa maoni yao na miongozo mbalimbali wanayoitoka kwa Shirika ambayo imeleta mafanikio makubwa mgodini hapo.

Kabla ya Ziara hiyo  ya Kiwira kamati iliweza kupata wasilisho la Utekelezaji wa Shughuli za Shirika tarehe 06.03/2025 Jijini Dodoma katika semina iliyoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Eng Yahya Samamba.

Katika semina hiyo kamati ililipongeza STAMICO kwa mageuzi makubwa yaliyofanywa na Shirika katika kipindi kifupi na kuwataka kuongeza juhudi  zaidi ili kuongeza mapato ya Shirika

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals