[Latest Updates]: Burundi Yapongeza Maendeleo Sekta ya Madini Tanzania

Tarehe : Dec. 11, 2024, 7:29 p.m.
left

BURUNDI YAPONGEZA MAENDELEO  SEKTA YA MADINI TANZANIA

Yapongeza maendeleo ya tafiti zilizofanyika

Dodoma

Ujumbe kutoka Burundi ukiongozwa na Mshauri wa masuala ya madini kutoka  Wizara ya Madini  nchini Burudi wafika Tanzania kujifunza namna bora ya Uongezaji Thamani Madini.

Ujumbe huo umefika leo Desemba 11, 2024 katika Ofisi za Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Jijini Dodoma na kukutana na Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo Dkt.Mussa Budeba pamoja na wataalamu mbalimbali.

Ujumbe huo ulipokelewa kwa wasilisho maalum kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Huduma za Jiolojia GSS, Yusto Shine  kuhusu hatua mbalimbali za maendeleo ya Sekta ya madini hususan katika  tafiti zilizofanyika pamoja na ugunduzi wa madini ambayo yanatoa mchango mkubwa kwa taifa na jamii kiuchumi.

Akizungumza kwa niaba ya Ujumbe  huo Mshauri wa masuala kutoka Ofisi ya Madini Burundi Niyongabo Regis ameipongeza Sekta ya madini nchini Tanzania kwa maendeleo ya tafiti zilizofanyika nchini ukiwemo utafiti wa Jiofizikia uliofanyika kwa asilimia 16, utafiti wa jiokemia asilima 24 na utafiti wa Jiolojia asilimia 97.

Niyongabo ameeleza kuwa, nchi ya Burundi bado ipo katika hatua mbalimbali za kuendeleza Sekta ya Madini  na Nishati katika kuunganisha kwenye mnyororo wa thamani kuanzia ngazi ya utafiti, uzalishaji mpaka katika masoko ya ndani na nje ya Burundi.

Niyongabo ameongeza kuwa kupitia Makubaliano ya Mashirikiano ya Kikazi (MoU), ambapo malengo ya Burundi ni kupiga hatua kama ilivyo Tanzania kwasababu inaaminika kuwa Maendeleo ni hatua na michakato ya mageuzi.

Awali, akiukaribisha ugeni, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa  Madini Tanzania (GST) Dkt. Mussa Budeba ameahidi kuendelea kutoa  ushirikiano wa kitaalam ambao utahusisha hatua zote za jiosayansi ikiwemo uchakataji wa taarifa za  ugani wa jiolojia, jiokemia, jiofizikia na uchapishaji wa ramani.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals