[Latest Updates]: Madini, Ufaransa Zajadili Kushirikiana

Tarehe : Feb. 15, 2024, 8:49 a.m.
left

Dodoma

Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Madini na Taasisi za  Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na Tume ya Madini  leo Februari 15, 2024 wamekutana na ugeni wa Kidplomasia kutoka Ubalozi wa Ufaransa nchini na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti ya Ufaransa  (BRGM).

Lengo la ugeni huo  lilikuwa ni  kutambua fursa za uwekezaji hususan  kwenye madini muhimu na mkakati  na  kuangalia maeneo ya ushirikiano  katika Sekta ya Madini nchini.

Katika kikao hicho kilichongozwa na Naibu Katibu Mkuu Msafari Mbibo, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba  amebainisha maeneo muhimu ya ushirikiano kuwa ni  pamoja  na uwekezaji katika  shughuli za utafiti wa kina wa madini na kuwajengea uwezo wanasayansi katika maeneo mbalimbali ya jiosayansi.

Masuala mengine yaliyogusiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wanajiosayansi kwenye masuala yanayohusu majanga ya asili ikichukuliwa mfano wa tukio la hivi karibuni lililotokea Wilayani Hanang la kumomonyoka kwa udongo na masuala yanayohusu akili bandia.

Akizungumza katika kikao hicho, Naibu Katibu Mkuu Mbibo ameueleza ujumbe huo kuwa bado ipo nafasi ya kukutana na kuendeleza ushirikiano baina yao na GST katika maeneo yaliyokubalika.

by: madini

Latest News
Biteko atoa wito Mabenki ya ndani kuungana kukope…

Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…

by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.

Ukusanyaji wa Maduhuli Sekta ya Madini Wafikia As…

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…

by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.

Aliyoyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Adol…

’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…

by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.

Tume ya Madini Yaagizwa Kutafuta Masoko

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…

by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.

Read News
Contact Us
Permanent Secretary,
Ministry of Minerals,
Madini Street,
Government City, Mtumba
P. O. Box 422,
Dodoma, Tanzania
Email: ps@madini.go.tz
Copyright©2021 Ministry of Minerals