Tarehe : April 20, 2023, 4:30 p.m.
Zikiwa zimepita takribani Siku 3 tangu Serikali ya Tanzania na Wabia kutoka Kampuni za Australia wasaini Hati ya Makubaliano ya Mikataba Mitatu ya uchimbaji Mkubwa na wa Kati kwa madini ya kimkakati, Aprili 20, 2023 Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Kheri Mahimbali na Balozi wa India nchini Binaya Pradhan wamekubaliana kushirikiana kuendeleza maeneo ya utafiti katika madini ya Kimkakati.
Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao kilichohudhuriwa na watalaam kutoka pande zote na kufanyika katika Ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar s Salaam.
Mbali na eneo hilo, pia nchi hizo zimekubaliana kushirikiana katika Sekta ya madini na kuendeleza utafiti wa jiofizikia kwa kutumia ndege (high resolution survey), kwa kushirikiana na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST).
Pia, makubaliano mengine ni kushirikiana katika mafunzo kwenye sekta ndogo ya uongezaji thamani madini hususan madini ya vito na kuendeleza rasilimali watu katika shughuli za uongezaji thamani madini.
Aidha, pande zote zimekubaliana kukamilisha taratibu za makubaliano hayo ili utekelezaji wa shughuli hizo uanze.
Makubaliano hayo ni matokeo ya jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali kupitia wizara ya Madini katika utekelezaji wa mikakati yake ikiwemo ya kufungua migodi ya uchimbaji mkubwa na kuweka msistizo katika uchimbaji wa madini ya kimkakati yakiwemo ya kinywe (graphite).
Aidha, mkakati huo unakwenda sambamba na juhudi za Wizara kuendelea kuhamasisha shughuli za uongezaji thamani madini ili zifanyike nchini kwa kuwawezesha vijana wengi wa kitanzania kupata ujuzi katika shughuli za uongezaji thamani madini pamoja na kuendelea kukiimarisha Kituo chake cha Jemolojia Tanzania (TGC) kinachotoa mafunzo ya uongezaji thamani madini ikiwemo ukataji na unga’rishaji wa madini ya vito, utambuzi na usanifu wa madini.
by: madini
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameyataka Mabenki ya ndani kushirikiana ili kuweza kuzikopesha kampun…
by: madini on: April 23, 2021, 5:11 a.m.
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa katika kipindi cha mwezi Julai, 202…
by: madini on: April 28, 2021, 12:51 p.m.
’Nimeona Nyuso Zenye Furaha , Amani na Utulivu’’ Ninayo furaha kuwa nanyi hapa ili tuanze safari hi…
by: madini on: Jan. 10, 2022, 2:55 p.m.
Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Tume ya Madini kutafuta Masoko ya wanunuzi wa…
by: madini on: Jan. 30, 2022, 9:32 a.m.